Tuesday, April 14, 2015

MAPYA YAIBUKA SHAMBULIO LA KIGAIDI GHARISSA

Mapya yaibuka  shambulio Chuo Kikuu Garissa Kenya..

Attack on Kenya's Garissa University CollegeFamilia za wanafunzi 142 kati ya  148 waliouawa katika shambulio la kigaidi la Al Shabaab kwenye Chuo cha Garissa Kenya wameruhusiwa kuchukua miili ya ndugu zao kwa ajili ya mazishi ambapo Serikali ililazimika kutumia mashine maalum kutambua baadhi ya miili ambayo iliharibika vibaya kutokana na majeraha ya risasi.
Hilo limeendelea lakini bado kuna ishu onawaacha watu njia panda,  zaidi ya wanafunzi 166 hawajulikani walipo, familia zao bado zimeendelea kulalamika kutokana na baadhi ya ndugu zao kutoonekana.
Uamuzi mwingine mgumu uliotangazwa na Kenya ni kulitaka Shirika la Wakimbizi UNHCR ndani ya miezi mitatu kufunga kambi ya wakimbizi  iliyoko mashariki mwa nchini hiyo pamoja na kuwarudisha kwao wakimbizi ambao ni raia wa Somalia zaidi ya laki nne.

No comments:

Post a Comment