Kingine kilichosikika kutoka Kenya kuhusu shambulio la Chuo Kikuu, kiongozi wa Serikali kahusishwa na uzembe..
Taarifa za kwenye vyombo vya
habari Kenya zinasema ndege ambayo ilitakiwa isafirishe maafisa wa
Polisi kwenda kwenye Chuo hicho kwa ajili ya kupambana na wavamizi hao
ilitumiwa kwa ajili ya safari binafsi ya familia moja ambapo kuna
kiongozi mmoja anahusishwa kuruhusu ndege hiyo kufanya safari hiyo
wakati ambao ilitakiwa kuwapeleka maafisa hao Garissa.
Rubani amesema ndege hiyo iliondoka
katika uwanja wa ndege na kuwaacha makomandoo wa RECCE wakisubiri irudi
kuwachukua na kuwapeleka Garissa kuwaokoa wanafunzi.
No comments:
Post a Comment