Tuesday, April 14, 2015

JAMAA AZINZIA NA KURUKA NA NDEGE SEHEMU YA MIZIGO

Jamaa alisinzia kwenye sehemu inayowekwa mizigo ndani ya ndege, kilichofuatia hapo ni ishu..

Alaska 737-700 WL N622AS (90)(Grd) SEA (MBI)(46)-M
Ishu ilianzia pale ambapo ndege ilikuwa imeruka kama dakika 14 hivi Uwanja wa Seattle, Marekani.. Rubani mmoja akahisi kwamba kuna mlio wa kitu tofauti toka kwenye sehemu ambayo inawekwa mizigo ndani ya ndege hiyo.
Marubani wa ndege hiyo ilibidi waombe dharura kuirudisha ndege uwanjani hapo kwa kuwa walihisi sauti ya kitu wanayoisikia toka kwenye chumba hicho cha mizigo itakuwa ni mtu.
alaska-airlines
Ndege hiyo ilipotua uwanja wa Seattle-Tacoma
Baada ya ndege hiyo kutua watu wa kitengo cha dharura waliingia ndani ya ndege na kumkuta jamaa amesinzia hana hata habari na kinachoendelea.
21.si
Mfanyakazi huyo alipotoka ndani ya ndege hiyo
Taarifa iliyotolewa na shirika la ndege hiyo imesema kuwa mfanyakazi huyo alipimwa lakini hakuwa ametumia kilevi chochote wala hakutumia dawa yoyote.. ndege hiyo aina ya Boeing 737, iliyokuwa na abiria 170 ilikuwa imeruka kwa dakika 14 angani ikielekea Los Angeles kabla ya kugundua kuwa kuna huyo jamaa ambaye alikuwa ammesinzia kwenye sehemu ya mizigo ya ndege hiyo.
  Hutopitwa na habari yoyote inyonifikia na nikon tayari kukutumia wakati wowotw kupitia hapa hapa www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment