Tangakumekuchablog
Muheza,WAKAZI
Wilayani Muheza Mkoani Tanga, wameitaka Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya,
kuisambaza Katiba Pendekezwa na kuwapa muda wananchi kuisoma kwa kina kabla ya
kuipigia kura.
Wakizungumza katika mkutano wa
hadhara ulioitishwa na Kituo cha
Sheria na Haki za Bianadamu (LHRC) uwanja wa soko la Tanganyika na kusema kuwa
Tume isambaze kila kaya Katiba
Pendelezwa na kuweza kusomwa kwa kituo.
Walisema kufanya hivyo kutawapa
nafasi wananchi siku ya kuipigia kura kujitokeza kwa wingi kwa kutambua
walichokisoma na kusema kuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya kuhakikisha kila
kaya imepata Katiba Pendekezwa.
“Unajua wengi tunasikia kuwa kuna
siku ya kuipigia kura katiba pendekezwa ila sie hatuijui wala kuiona-----itatuwia
vigumu kupiga kura kitu ambacho hatukijui” alisema Michael Mhina
“Ili kuliwezesha jambo hili ambalo
niko na maslahi na wananchi ni vyema tume ya mabadiliko ya katiba mpya
kuisambaza katiba pendekezwa kila kaya na kuwapa nafasi wananchi kuisoma”
alisema
Awali akiwahutubia wananchi,Mratibu
wa zoezi la kutoa elimu ya uraia Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC),
Stanley Humbo, amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi wakati wa kuipigia kura
Katiba Pendekezwa.
Amesema ni haki ya kila mtu kuchukua
maamuzi sahihi ya kuipigia kura Katiba Pendekezwa kwani maoni yake ndio ambayo
yatazaa kupatikana kwa Katiba Mpya
ambayo kwa muda mrefu ilikuwa ikilalamikiwa kwa baadhi ya mambo.
Amesema maoni hayo yatakayowezesha kupatikana Katiba Mpya ambayo kwa muda mrefu
wananchi walikuwa wanaisubiria ikiwa na pamoja na kuondosha manung’uniko kwa
baadhi ya mambo yaliyomo.
“Ndugu zangu wa Muheza ni wajibu wa
kila mmoja kujitokeza siku ya kuipigia kura katiba pendekezwa kwani iko na
maslahi na wananchi na Taifa kwa ujumla” alisema Humbo
Alisema Katiba hiyo Pendekezwa
itagawiwa na kila mmoja kuisoma kwa nafasi na hivyo kuwataka kujitokeza kwa
wingi siku ya kuipigia kura na kuweza kupata Katiba mpya ambayo itatuongoza kwa
miaka mingi.
Wakazi wa Muheza Tanga wakisikiliza elimu ya elimu ya upigaji kura Katiba Pendekezwa iliyotolewa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) mkutano uliofanyika viwanja vya soko la Tanganyika
Wakazi wa Muheza Tanga wakisikiliza elimu ya upigaji kura Katiba Pendekezwa iliyokuwa ikitolewa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) mkutano uliofanyika uwanja wa soko la Tanganyika






No comments:
Post a Comment