Wednesday, April 15, 2015

AJALI KILA KONA, NI VILIO TU

BASI LA GAMET TRANS LAPATA AJALI, LEO

Basi la kampuni ya GAMET Trans linalofanya
safari zake Dar-Lindi-Masasi-Nachingwea limepata ajali  maeneo ya Kibiti
Wilaya ya Rufiji-Utete Mkoa wa Pwani baada ya kutaka kumkwepa mtu
anayedaiwa kuwa na tatizo la ulemavu wa akili,lakini kwa bahati mbaya
likamgonga na kufariki papo hapo,taarifa zaidi zinaeleza kuwa baada ya
ajali hiyo basi hilo liliacha njia na kupinduka na kupelekea kifo cha
mtu mmoja aliyegongwa na wengine waliokuwemo ndani ya basi hilo .


Basi la kampuni ya GAMET Trans linalofanya safari zake Dar-Lindi-Masasi-Nachingwea likiwa limepinduka na majeruhi wa ajali hiyo wakipatiwa msaada na wasamaria wema.

Basi la kampuni ya GAMET Trans linalofanya safari zake Dar-Lindi-Masasi-Nachingwea likiwa limepinduka kama linavyonekana katika muonekano hapa. 

No comments:

Post a Comment