Msichana kamkataa mpenzi wake, eti nd’o akataka kumuua?
Msichana huyo amesema mpenzi wake huyo alimfuata nyumbani kwake na kumnywesha kwa nguvu maji ya betri kwa lengo la kumuua.
Dada wa msichana huyo amesema alitumiwa
message na mwanaume huyo kwa kutumia simu ya mdogo wake, akimtaarifu
kuwa hajui kama mdogo wake ni mzima au amefariki, dada huyo
akaamua kufuatilia na kukuta mdogo wake amepelekwa Hospitali ya
Mwananyamala huku akiwa kwenye hali mbaya.
Chanzo cha ugomvi wanasema ni ishu ya
msichana huyo kumkataa mwanaume baada ya kugundua kuwa ana mke.. siku ya
tukio mwanaume huyo alimfuata nyumbani kwake, akamlazimisha kuingia
ndani na kuaanza kumkaba huku akimnywesha maji ya betri.
Baadae mwanaume huyo alikimbia lakini
bado ameendelea kuwatumia ujumbe wa kuwataarifu kuwa atahakikisha
anamuua msichana huyo na yeye atajiua.
No comments:
Post a Comment