Wednesday, November 11, 2015

HAPA NI KAZI TU, RAIS MAGUFULI AZIDI KUWAPA MATUMAINI WATANZANIA

Kilichonifikia kuhusu mashine za MRI kutoka hospitali ya Muhimbili…

Siku ya tatu baada ya Rais Dk Magufuli kuingia Ikulu na kuanza kazi alifanya ziara za kushtukiza katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili ikiwa ni baada ya kumaliza ziara katika Wizara ya Fedha siku moja baada ya kuapishwa.
Baada ya kutembelea hospitali ya Muhimbili alifanya mabadiliko ikiwa kumsimamisha kazi Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali hiyo Hussein Kidantu sambamba na kutaka mashine za CT Scan na MRI zifanyiwe ukarabati baada ya kukaa miezi miwili bila kuhudumia wagonjwa kutokana na ubovu wake.
Kamati mpya tendaji ya hospitali hiyo ilikutana jana na mara moja kuitisha wataalam ambao leo walianza kazi ya utengenezaji wa mashine hizo.
Taarifa mpya kutoka kwa Mkuu wa kitengo cha mawasiliano ya umma Aminiel Eligaisha amesema ni kweli mashine za MRI tayari zimeanza kufanya kazi na mashine za CT Scan bado zipo katika matengenezo na zitaanza kufanya kazi wakati wowote kuanzia sasa.
Barua ilisomeka hivi…
barua

Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment