Thursday, October 12, 2017

HADITHI, MBIO ZA SAKAFUNI HUISHIA UKINGONI SEHEMU YA 13

HADITHI hii inaletwa kwenu kwa hisani kubwa ya Kampuni ya mabasi ya abiria FREYS LUXURY COACH, ifanyayo safari zake kati ya Tanga hadi Sindida kila siku kupitia Moshi, Arusha na Babati, na hufanya hivyo kila siku kutokea Singida kwenda Tanga kupitia Babati, Arusha, Moshi hadi Tanga, kwa mawasiliano, 0622 292990

MBIO ZA SAKAFUNI HUISHIA UKINGONI 13

ILIPOISHIA

Polisi hao wakaanza kupima ajaIi hiyo na kuzuia magari mengine yapite kando. Baada ya kupima ajali polisi mmoja alimwambia dereva wa gari jingine atoe kadi ya gari lake.

“Iko nyumbani” aliwambia.

“Kwanini hutembei nayo?”

“Niliisahau”

“Leseni yako iko wapi?”

Jamaa alijipapapasa kisha akasema.

“Leseni pia nimeisahau nyumbani”


SASA ENDELEA
“Kila kitu Umesahahu nyumbani? Yaani unaendesha gari bila kuwa na leseni?”

“Sio kama sina, nimeisahau tu”

“Tutaaminije kama unayo leseni au huna?”

“Nitakwenda kuichukua”.

Kombo alikuwa yuko ofisini kwake akisubiri ruhusa ya kurudi tena nyumbani kwa Waziri Mkuu kumhoji kuhusu utata uliojitokeza kati ya maelezo yake na maelezo ya Mzee Amrani, simu yake ikaita juu ya meza.

Aliunyakua mkono wa simu na kuuweka sikioni kwake, akasema.

“Hello!”

“Kuna gari limekamatwa na polisi wa usalama barabarani limefanana na lile lililoshukiwa, ni aina ya Land Cruiser la rangi nyeupe. Nimewaambia walilete hapa” Kombo aliitambua sauti hiyo kuwa ilikuwa ya afisa upelelezi.

“Limekamatwa wapi?” Kombo akauliza.

“Limekamatwa Kimara, liligongana na gari jingine lakini limegundulika kuwa ni la waziri mkuu”

“Ni nani aliyekuwa akiliendesha?”

“Ni dereva wake”

“Ningependa nimuone”

“Hilo gari litaletwa sasa hivi pamoja na huyo dereva”
                                                                  
                                       *******

Waziri Mkuu alikuwa amesharudi nymban kwake alipopigiwa simu na dereva wake Kidasi Athumani.

“Mzee nimepata ajali, gari limekamatwa na polisi” Kidasi alimwamba Wazri mkuu kwenye smu.

“Umegonga au umegongwa?”

“Nimegonga gari kwa nyuma. Gari lilifeli breki”

“Kuna aliyejeruhiwa?”

“Hakuna aliyejeruhwa”

“Ajali imetokea wapi?”

“Kmara. Nilikuwa narudi kutoka Kibaha”

“Ilikuwa ajali kubwa?”

“Si kubwa lakini gari nililoligonga limebonyea kwa nyuma”

“Polisi wamekwambia nini?”

“Wamenikamata”

“Umewambia kuwa gari hilo ni langu?”

“Nmewambia”

“Sawa. Waache wafuate taratibu zao halafu utanifahamsha”

“Sawa mzee”

Waziri Mkuu aliiweka simu yake juu ya meza kisha akamtazama mke wake.

“Kidasi amepata ajali” akamwambia.

“Wapi?”

“Kimara”

“Amegonga au amegongwa?”

“Amegonga”

Mke wa Wazir Mkuu akaguna.

“Wiki hii ni ya mkosi kwetu, sijui ni kitu gani kinataka kututokea”

“Yuko kituo cha polisi, nimemwamba anifahamishe kitakachoendelea. Kama mwenye gari atataka kulipwa tutamlipa, kama atataka tuendelee na kesi sawa”

“Vizuri ni kumlipa tu”

“Akitaka tumlipe gharama za matengenezo tutamlipa”

“Kabla ya Kidasi kukupigia simu ulikwa unataka kunieleza kitu”

“Nimearifiwa kuwa wale wapelelezi wanataka kurudi tena kutuhoji kuhusu kuuawa kwa Pili”

“Waje tena mara ya pili?“

“Ndio, na mimi nimeshangaa”

“Labda wamegndua kitu”

“Kitu gani?”

“Kitu chochote tu. Unadhani wanakuja bure”

“Nmewambia na waje tu”

“Watakuja saa ngapi?”

“Nimewambia baada ya masaa mawili nitakuwa nyumbani. Wanaweza kuja wakati wowote kutoka sasa”

                              *************

Kidasi alishangaa alipoona akipelekwa katika ofisi ya idara ya upelelezi makao ya polsi. Aliingizwa katika ofisi Thabit Kombo na kuanza kukabiliana na maswali ambayo hayakuhusiana na ajali iliyotokea.

“Wewe upo katika ajira ya serikali au binafsi?” Kombo alimuuliza.

“Niko katka ajira binafsi. Waziri Mkuu aliniajiri niwe dereva wa gari zake”

“Gari zake binafsi sio?”

“Ndio”

“Unamuendesha nani?”

“Zile gari ni kwa ajili ya shughuli za shamba lake lililoko Kibaba”

“Sawa. Ni wakati gani unaingia kazini, na wakati gani unatoka kazini?”

“Sina muda maalum wa kuingia au kutoka kazini. Kuna siku naingia kazini saa kumi na moja alfajir kwa ajili ya kwenda Kibaha kufuata maziwa ya ngombe. Ninakuwa kwenye gari nyengine. Siku nyngine naingia kazini saa mbili asubuhi”

“Na kutoka?”

“Pia sina muda maalum, inategemea nitakapomaliza kazi ninazotumwa”

“Unaweza kuwa na gari hilo hadi saa ngapi?”

“Wakati mwingine hadi saa nne usiku”

“Hebu niambie jana ulitoka saa ngapi kazini?”

“Nilitoka saa nne usiku”

“Ulikuwa umekwenda wapi?”

“Kibaha”

“Na uliondoka hapa jijini saa ngapi?”

“Niliondoka saa kumi”

“Hilo gari liko wapi?”

“Limeletwa hapa makao ya polisi”

“Hebu twende nikalione”

Kombo na Kidasi walitoka ofisini wakaenda lilikokuwa gari hilo.

Kombo alilikagua. Alifungua mlango wa nyuma na kulitazama ndani kisha akafunga mlango.

“Kwa hiyo jana ulikuwa na gari hili hadi saa nne usiko?”

“Hili gari nilikuwa nalo kuanzia asubuhi hadi saa kumi ambapo nilichukua gari jingine ambalo tunabebea ndoo za maziwa”

“Sio hili?”

“Hapana. Kuanzia saa kumi hadi saa nne usiku nilikuwa na gari jingine, sio hili”


itaendelea kesho usipitwe na uhondo huu hapahapa tangakumekucha

No comments:

Post a Comment