HADITHI
MBIO ZA SAKAFUNI HUISHIA
UKINGONI 18
ILIPOISHIA
“Ungeweza kuitimiza nadhiri
yako na hilo
tatizo lingeondoka lakini sasa kuna tatizo jingine”
“Tatizo gani?”
“Ule mzimu haupo tena, ni
afadhali kama ungehamishwa na kupelekwa sehemu
nyingine lakini aliondolewa kabisa. Na hivi sasa haupo tena”
Waziri Mkuu akakumbuka amri
ya kuuondoa mzimu huo kwenye kijiji hicho aliitoa yeye baada ya kuona kijiji
kilikuwa kimepanuka na watu walikuwa wakifanya vitendo vya kishirikina waziwazi na kusababisha fisi
waliokuwa wakifuata mizoga ya wanyama kuhatarisha maisha ya watu.
“Ni bora ningeuacha” Waziri
Mkuu akajiambia kimoyo moyo.
“Sasa kama huo mzimu haupo
haitawezekana kutimiza ile nadhiri?” akauliza huku akiizuia sauti yake
isioneshe hofu.
“Haitawezekana. Mzimu wenyewe
haupo. Hiyo nadhiri utaitimiza wapi?”
Waziri Mkuu akamkumbuka
mwanawe.
“Sasa mwanangu atapona vipi?”
“Hilo swali ni vigumu kukujibu, ungemfuata
yule mganga wa kwanza uliyekwenda naye kwenye huo mzimu”
SASA ENDELEA
“Nimeambiwa huyo mganga
amekwishakufa”
Mganga akatikisa kichwa
kusikitika.
“Hilo
suala litakuwa gumu sana”
“Una maana gani, una maana
kwamba mwanangu hatapona”
Mganga aliendelea kutikisa
kichwa.
“Kupona itakuwa vigumu sana”
Waziri mkuu alitoa macho ya
taharuki.
“Unasemaje?”
“Mheshimiwa kwa upande wangu,
sina uwezo wa kukusaidia” Mganga akasema huku uso wake ameuinamisha chini
akiyakwepa macho ya mheshimiwa.
“Unadhani nani anaweza
kunisaidia?”
“Sijui lakini unaweza
kujaribu kwa waganga mbalimbali”
“Loh! Itakuwa ni kazi!”
“Hakuna njia nyingine ya
kufanya isipokuwa kuhangaika tu, kujaribu huku na huku”
“Namsikitikia sana mwanangu na ninajuta
kuweka ile nadhiri”
“Na ni kwanini uliweka
nadhiri halafu ulishindwa kuitimiza katika muda wake?
“Kusema kweli sikudhani kama yangekuwa makubwa kiasi hiki”
“Umedharau
kitu ambacho hukijui. Ni bora usingekwenda kuweka nadhiri ile”
“Yaani ninajuta..!”
Palipita kimya cha karibu
nusu dakika kabla ya mganga huyo kuinuka na kumuaga Waziri Mkuu aliyekuwa
amechanganyikiwa
“Mheshimiwa naona
nikuage…ninakwenda zangu”
“Ehe! Ndio unakwenda?” Waziri
Mkuu akamuuliza baada kuzinduka kwenye mawazo.
“Naona niende, kuna kazi
zinaningoja”
Waziri Mkuu naye akasimama.
Hisia za uheshimiwa zilikuwa zimeshamtoka.
“Sasa utanisaidiaje?”
“Labda nijaribu kukuulizia
kwa wataalamu wengine.
“Basi jaribu kufanya hivyo,
nitakupa zawadi yako. Utakuwa unawasiliana na huyu ndugu yangu anayeishi hapa”
“Sawa. Kama nikifanikiwa
kupata mtu anayeweza kulitatua hilo
tatizo nitamfahamisha”
“Asante
sana”
Wakapeana mikono kuagana.
Mganga akatoka. Waziri Mkuu
alirudi kwenye kochi
akaketi na kukiinamisha kichwa chake.
Ndugu yake akaingia na kuketi
kando yake.
Waziri Mkuu akamtazama.
“Nina matatizo makubwa ndugu
yangu, inabidi nikueleze lakini hii iwe ni siri yako” akamwambia.
“Itakuwa ni siri yangu, ni
matatizo yapi kaka?”
Waziri Mkuu akamueleza tatizo
la mwanawe na jinsi waganga walivyomueleza kuwa lilitokana na mizimu.
“Niliwahi kuweka nadhiri
kwenye ule mzimu ulioondolewa halafu sikutimiza nadhiri ile” alimwambia.
“kwa hiyo huo mzimu ndio
umemuingia binti yetu?”
“Ndivyo ninavyoambiwa na
wataalamu na inaweza kuwa ni kweli kwa sababu vipimo vyote vya hospitali
vimeonesha kuwa Sofia
hana matatizo”
“Sasa huwezi kuitimiza hiyo
nadhiri kwa sasa?”
“Haiwezekani kwa sababu ule
mzimu haupo tena”
“Huyu mganga niliyemleta
amekushauri nini?”
“Ameshindwa”
“Tutatafuta waganga wengine,
wapo wengi”
“Basi nitafutie, itabidi
nirudi Dar muda huu lakini ukimpata
nipigie simu nitakuja mimi au mke wangu”
“Hakuna tatizo kaka,
nitafanya kazi hiyo”
Waziri Mkuu akarudi Dar.
Asubuhi ya siku iliyofuata kabla ya kutoka kwenda ofisini kwake ndugu yake
akampigia simu.
“Asubuhi njema kaka” Sauti
kutoka simu ya upande wa pili ikasikika.
“Na kwako pia. Mmeamka salama
huko?”
“Sisi tumeamka salama, sijui
nyinyi huko?”
“Huku pia tumeamka salama. Umeshughulikia lile suala langu?”
“Nimelishughulikia jana ile
ile na nimepta mtu ambaue ataweza kutusaidia”
Waziri Mkuu alijisikia kupata
nguvu ndani ya kiwiliwili chake.
“Kweli eh!” akauliza.
“Sasa sijui utakuja lini
huku?”
“Umemueleza
hali halisi ilivyo?”
“Nimemueleza kila kitu na
nimemueleza kuwa ule mzimu kwa sasa haupo tena. Ameniambia uje”
“Atakuja mke wangu pamoja na
huyo binti”
“Atakuja lini?”
“Atakuja leo hii”
“Saa ngapi?”
“Sijaua saa lakini
watakapokuja nitakufahamisha”
“Sawa, basi nawasubiri”
Wakati ule mheshimiwa Waziri
Mkuu alikuwa chumbani kwake akatoka haraka na kwenda sebuleni ambako mke wake
alikuwa akizungumza na Sofia.
“Hebu njoo chumbani”
akamwambia.
Mke wake alimuacha Sofia akamfuata mume wake
chumbani.
“Kuna nini?”
“Stambuli amenipigia simu
ameniambia yule mtaalamu atakayeweza kuyashughulikia haya matatizo amepatikana,
sasa nataka uende Morogoro na Sofia
baada ya kumaliza kazi zako”
“Naweza kuacha kazi zote ili
niende naye”
“Basi fanya hivyo, mimi
naenda ofisini”
“Wewe nenda, tukitoka
nitakupigia simu”
“Sawa”
Dakika chache baadaye akiwa
ofisini kwake Waziri Mkuu akapigiwa simu na mke wake.
“Ndio tunatoka”
“Sawa. Nataka huyo dereva
wako asijue kitu”
“Hatajua”
“Unijulishe kitakachoendelea”
“Nitakujulisha”
Mke wa waziri Mkuu alifika
Morogoro katika kijiji alichotoka mume wake.
Shemeji yake Stambuli baada
ya kumkaribisha nyumbani alimwambia asubiri ili aende akamchukue huyo mganga
aliyezungumza naye.
Aliondoka kwa gari lake kuelekea
alikokuwa akiishi mganga huyo ambako kulikuwa kijiji cha pili
Alipofika alimkuta mganga
huyo akihudumia mtu. Akamsubiri hadi alipomaliza, alimfuata na kumwambia kuwa
mke wa Waziri Mkuu pamoja na binti yao
mwenye matatizo walikuwa tayari wamefika nyumbani kwake.
Mganga huyo kwa heshima ya
kumhudumia binti wa Waziri Mkuu alijiandaa haraka haraka akajipakia kwenye gari
ya Stambuli wakaondoka.
Walipofika kwa mke wa Waziri
Mkuu, Stambuli aliwapisha. Sofia
pia hakutakiwa kusikiliza yale mazungumzo.
ITAENDELEA kesho Usikose kuwa nami hapahapa tangakumekuchablog
UTAJIRI AU FEDHA ZA NDAGU AU MAJINI KWA MUDA MFUPI MPAKA MASAA 48(Siku 2) POPOTE ULIPO.
ReplyDelete(Kwanza kabisa nataka kukwambia kwamba hakika utajili ni azina kutoka kwa mwenyezi mungu na pia kuna viumbe alio wapa mamlaka na nguvu ya kumiliki mali)
MPAKA MASAA 72(SIKU3) PAPO HAPO KWA MASHARTI MAALUM KIKUBWA UWE MWAMINIFU, JASILI NA UWE NA UTAYARI WA KUPOKEA MASHARTI YA KUTUNZA SIRI HII SIO MZAHA......
KUMBUKA MALIPO NI BAADA YA KUFANIKIWA
kwa maelezo kamili piga namba +255742162843
(KWANINI USUMBUKE,HACHA KUTANGATANGA, NA MAISHA NI MAFUPI PUUZA UONGOFU WA KUWA MTU KUWA TAJIRI NI DHAMBI WAKATI AKUAMBIAE YEYE NI TAJIRI (Tumia ufahamu kujinasuaUTAJIRI WA NDAGU(MASHARTI) NDANI YA MASAA 72(SIKU TATU) PAPO HAPO KIKUBWA UWE MWAMINIFU, JASILI NA UWE NA UTAYARI WA KUPOKEA MASHARTI YA KUTUNZA SIRI HII SIO MZAHA......
KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO TUNAPITIA MENGI ILI TUWEZE KUFANIKIWA LAKINI WENGI WETU KUNA MAMBO MACHACHE SANA WENGI WETU TUNAYADHARAU NA KUMBE NDIO CHANZO CHA MAFNIKIO YETU.
NAITWA DR, MDIRO piga 0742162843. KAMA UNAITAJI PESA ZA MAJINI AU NDAGU YA MALI AU ULINZI KWA MALI YAKO
(HUSITUME SMS PIGA SIMU KUHEPUKA MATAPELI)
MATIBABU MENGINEYO NI KAMA UTULIVU KATIKA NDOA, AU KUMVUTA UMPENDAE, KUONDOA MIKOSI, MABALAA, KUOSHA NYOTA, KUITAMBUA NYOTA YAKO NA ASILI YA KAZI YAKE, KAMA UNASUMBULIWA NA MAJINI MAHABA NA SHIDA YA UZAZI.
NIPIGIE 0742162843. KIKUBWA NI KUSIKILIZA NA KUFATA MASHARTI. ANGALIZO USITUME SMS PIGA NA UWE NA NIA.
(kuhusu utajiri au pesa) KABLA YA KUPIGA SIMU ZINGATIA YAFUATAYO
1. uwe una umri wa miaka 18+
2. uwe tayari kupokea masharti yote
3.uwe na uwezo wa kutunza siri
4. uwe jasiri wa kupokea taarifa yoyote
KARIBU SANA KWA SHIDA NYINGINE PIA ULIYONAYO
SAFARI YAKO YA MAFANIKIO UTAJIRI NA RIZIKI ZAKO ZIMESIMAMA NA KUZINASUA UWEZE KUSONGA MBELE SOMA KWA UMAKINI UWEZE KUIJUA SIRI HII.
HAYA NI MAMBO 7 YAKUZINGATIA KATIKA SAFARI YAKO YA MAFNIKIO
i) Wazazi wako wakiwa wamekulea mpaka ukawa mkubwa wafumbua macho unawaona akikisha usiwafanye wakajuta kukuzaa asilimia kubwa wazazi wanakuwa na tabu sana ila zile tabu zao ndio zinazokufanya wewe una aminiwa na watu na unaeshimika na kujieshimu
Kwaiyo jitahidi sana kuwa nao vizuri kuna wengi maisha yao wanaishi kwa shida chanzo ni utofauti baina ya wazazi wao
Ukiona wazazi wako wanatabu sana usiwajibu vibaya wewe kaa nao mbali ila wape majukumu yao unacho fanya kuwaona nakurudi ulipo apo utaona mambo yako yatakuwa vizuri sana
ii) JAMBO LA PILI
Akikisha unatunza uzao wako yani ukijua ni mtoto ni wako basi jitahidi sana kutoa uduma ata kidogo ulicho nacho lakini udumia usiache uzao wako unateseka na njaa wewe una kula maisha aisee fahau
Kila mtoto wako anavyo kuwa ndio mambo yako yanaaribika usipo udumia kwaiyo ukiwa waitaji kufanikiwa zaidi jali uzao wako
iii) JAMBO LA TATU
ukiwa umeoa au umeolewa usitoe talaka au kuomba talaka kabla mwenzio ayupo tayari kwa muda huo fahamu ukiomba talaka au akikupa talaka bila bila sababu ya msingi yeye tu ana matamanio ya kidunia basi anamuda atapoteza muelekeo wa maisha yake
iv) UKIWA WAPATA PESA
ukiwa wapata pesa alafu utoi sadaka basi kufikia kwenye ukuu utachelewa sana mana mana pesa badala ya kutoa kwa iyari yako utatoa kwa matatizo kwaiyo jitahidi icho icho kidogo toa sadaka kwa wenye uitaji
v) USIMZULUMU MTU
kama wataka kufika mbali kwenye mafanikio yako usimzulumu mtu ata kwa uchache wa kitu usifanye ivyo itakugarimu kiasi kikubwa
vi) USIZARAH MILA
ukiwa kwenu kuna mambo ya mila mzimu tambiko jitahidi kufatilia sana aya mambo yanarudisha nyuma sana usipo yawahi mapema
vii)USIWE WA NAMNA
1)ikiwa ujafanikiwa jitahidi sana usiwe mvivu kufanya kazi usiwe muhuni usiwe mwenye chuki na asira zisizo za msingi usiwe na tamaa nyoa vizuri vaa nguo za eshima na usiige maisha ya watu.
KWA MAWSILIANO ZAIDI KUHUSU MATATIZO MBALIMBALI YA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA, PETE MALI ZA NDAGU NA MAJINI N.K
DOKTA MDIRO Call/whatsup +255 742162843.