Tuesday, October 3, 2017

HADITHI, MBIO ZA SAKAFUNI HUISHIA UKINGONI SEHEMU YA 3

HADITHI

MBIO ZA SAKAFUNI HUISHIA UKINGONI 3

ILIPOISHIA

Hospitali yenyewe ilikuwa Masaki. Ilikuwa hospitali kubwa ya binafsi iliyokuwa ikiendeshwa na mzalendo wa Kitanzania. Ilikuwa ikitumiwa zaidi na mawaziri na waheshimiwa wengine ndani ya serikali.

Baada ya uchunguzi uliochukua dakika kadhaa kutoka katika sampuli ya damu ya binti wa Waziri Mkuu, iligunduliwa kuwa binti huyo hakuwa akisumbuliwa na malaria.

Madakatari walichukua vipimo vingine ambavyo navyo vilionesha kuwa Sofia hakuwa na tatizo lolote la kiafya.

Matokeo hayo licha ya kuutuliza moyo wa Sofia, yalimshangaza mama yake. Sofia alipoulizwa anajisikiaje alijibu kuwa alikuwa anajisikia vizuri.

“Alisema kichwa kilikuwa kinamuuma sana” Mama yake akawambia madaktari.

“Lakini sasa hivi hakiumi tena” Sofia akadakia.

“Anaonekana kuwa na afya njema. Uchovu pia unaweza kusababisha kuumwa kichwa. Hili si tatizo kubwa hasa kama linatokea kwa mara moja” Daktari alimwambia mama yake Sofia.

SASA ENDELEA

Sofia hakupata matibabu yoyote akarudishwa nyumbani. Dereva alipewa shilingi elfu hamsini na waziri kwa ajili ya usafiri wake kabla ya kuondoka.


“Ninashanga kusikia kuwa Sofia hana malaria” Waziri alimwambia mke wake akiwa chumbani.

“Hata mimi nimeshangaa na mwenyewe anasema anajisikia vizuri”

“Sasa amepatwa na tatizo gani?”

‘Inabidi tuendelee kumfanyia uchunguzi zaidi”

“Okey, sasa hili suala jingine tutalitatua vipi?”

“Sijui wewe mwenzangu umewaza nini?”

“Kusema kweli kichwa changu kimevurugika sana. Ni afadhali ingegundulika kuwa Sofia ana malaria”

“Itaonekana kwamba aliua kwa kukusudia”

“Lakini ni lazima kutakuwa na tatizo, Sofia hawezi kumtoboa mtu na kumfyonza damu hadi kumuua”

“Na inaonekana alifanya hivyo bila kujielewa”

“Kwa hiyo ni lazima kuna tatizo”

**************

“Ninashangaa kusikia kuwa Sofia hana malaria” Waziri alimwambia mke wake wakiwa chumbani.

“Hata mimi nimeshangaa na mwenyewe anasema anajisikia vizuri”

“Sasa amepatwa na tatizo gani?”

‘Inabidi tuendelee kumfanyia uchunguzi zaidi”

“Okey, sasa hili suala jingine tutalitatua vipi?”

“Sijui wewe mwenzangu umewaza nini?”

“Kusema kweli kichwa changu kimevurugika sana. Ni afadhali ingegundulika kuwa Sofia ana malaria”

“Itaonekana kwamba aliua kwa kukusudia”

“Lakini ni lazima kutakuwa na tatizo, Sofia hawezi kumtoboa mtu na kumfyonza damu hadi kumuua”

“Na inaonekana alifanya hivyo bila kujielewa”

“Kwa hiyo ni lazima kuna tatizo”

“Sasa tatizo limezaa tatizo na tunatakiwa tulishughulikie usiku huu huu”

“Sikiliza mke wangu, siwezi kumtia binti yangu kwenye matatizo ya kiserikali, si unajua tuhuma za mauaji ni kubwa. Na pia siwezi kujitia mimi mwenyewe katika matatizo ya kiserikali, bado ninahitaji niwe waziri mkuu kama nilivyo, nisingependa nipate kashfa yoyote”

“Umekusudia kufanya nini”

“Hili tatizo limetokea kwa bahati mbaya na linaweza likatuweka mahali pabaya sisi sote. Kwa hiyo nimeona nifanye kitu kimoja”

“Kitu gani?”

“Si kitu kizuri lakini ni lazima nikifanye haraka iwezekanavyo ili kuokoa jahazi”

“Ningependa kukisikia ili tushauriane”

“Nataka niuchukue huu mwili wa Pili nikautupe sehemu nyingine usiku huu”

“Ukishautupa itakuwaje?’

”Ninataka ionekane kuwa Pili hakuuawa nyumbani kwangu”

“Ni wazo zuri…”

“Mwili wake utakapoonekana asubuhi nitaeleza kuwa Pili aliondoka nyumbani kwangu saa moja usiku. Alituambia kuwa anaumwa na kichwa na alitumia usafiri wake mwenyewe”

“Ni sawa. Katika kujinusuru mpango huo unafaa”

“Sidhani kama kuna mtu atatushutumu”

“Si rahisi”

“Polisi watachunguza na wataona ameuawa na watu wengine”

“Mimi nakubaliana na wazo hilo”

“Sasa kama tumekubaliana acha nibadili nguo, niubebe ule mwili niutie kwenye gari langu. Nitaendesha mwenyewe. Ile gari yangu binafsi haijulikani sana, hakuna atakayeweza kunitambua”

“Halafu utakwenda kumtupa wapi?”

“Nitatafuta sehemu yenye kiza mitaa ya uswahilini. Hakuna atakayeniona usiku huu’

“Kwani hivi sasa ni saa ngapi?”

Waziri aliitazama saa yake ya mkononi.

“Sasa ni saa tano, inakaribia kuwa na robo”

“Bado ni mapema mno, ungesubiri angalau ifike saa saba. Kutakuwa kimya sana”

“Kusubiri hadi saa saba ni kupoteza muda, huu mwili tunatakiwa tuuondoe haraka humu ndani. Sidhani kama nitakosa sehemu nzuri muda huu”

“Sawa, basi wahi”

Waziri akabadili nguo. Alivaa jinzi na tisheti. Kichwani alivaa pama ili kuficha uso wake.

“Umebadilika sana” mke wake alimwambia na kuongeza.

“Si rahisi mtu kukutambua”

“Na kwa vile nitatumia gari langu binafsi ndio sitatambulika kabisa”

“Sasa twende tukasaidiane kumbeba”

Wakatoka chumbani. Walikwenda stoo wakauchukua mwili wa msichana huyo na kutoka nao. Waliupakia kwenye gari la waziri katika siti ya nyuma.

Waziri akafungua mlango wa dereva akajipakia na kuliwasha gari.

“Ngoja niende” alimwambia mke wake na kulitoa gari.

Kwa saa kadhaa Waziri Mkuu alikuwa akizunguka na gari lake katika mitaa ya eneo la Kinondoni ambako Pili, msichana aliyeuawa na mwanawe alikuwa anaishi.

Waziri Mkuu hakuwa akijua Pili alikuwa akiishi katika mtaa gani lakini hilo halikuwa tatizo kwake. Mradi alikuwa akijua kuwa alikuwa akiishi katika eneo hilo alitaka kuuacha mwili wake mahali popote tu ili iwe rahisi kutambuliwa na ndugu na jamaa zake.

Ingawa ulikuwa usiku mwingi baadhi ya mitaa ya eneo hilo ilikuwa bado ina harakati za watu. Baadhi ya mitaa mengine iliyokuwa iko kimya ilikuwa imeng’arishwa na taa za barabarani pamoja na taa za majumbani, hali iliyosababisha waziri ashindwe kuutelekeza mwili huo aliokuwa ameupakia kwnye gari.

Katika kuzunguka zunguka kutafuta sehemu tulivu iliyo kimya na yenye kiza alitokea katika eneo la shule moja ya msingi ambayo ilikuwa na kiwanja cha mpira.

Kiwanja hicho kilikuwa kama jangwa lililoachwa pekee. Karibu na kiwanja hicho kulikuwa na majengo ya shule yaliyokuwa kiza na kimya.

Waziri akaona mahali hapo palikuwa muafaka kuuacha mwili wa Pili kwani hapakuwa na nyumba za watu karibu na palikuwa kiza. Aliliingiza gari ndani ya eneo la kiwanja hicho akavipita kidogo vyuma vya magoli ya upande mmoja kisha akalisimamaisha gari.

Alibaki kwenye siti kwa dakika kadhaa kuangalia kama kutatokea mtu yeyote. Alipoona hakukuwa na mtu yeyote aliyejitokeza akafungua mlango wa gari na kushuka.

Alikwenda kwenye mlango wa siti ya nyuma akaufungua. Aliuvuta mwili wa Pili akautoa kwenye gari. Akiwa ameushikilia mikononi alikwenda pembeni mwa goli, mahala ambapo palikuwa na mti wa mwembe.

Alitaka auweke mwili huo chini ya mwembe uliokuwa hapo lakini ghafla akashitushwa na mwanga wa tochi uliokuwa ukimmulika. Mwanga huo ulitokea sambamba na mlio wa mabuti uliosikika kutoka nyuma yake.

Ule mshituko uliufanya mwili wake usisimke. Akiwa bado ameushikilia mwili wa Pili aligeuka haraka na kutazama nyuma.

“Wewe nani na unafanya nini mahali hapo?” Sauti nzito ya mtu aliyekuwa akija kwa haraka nyuma yake ilimtatanisha.

Akagundua mara moja kuwa alikuwa mlinzi wa ile shule. Alikuwa amevaa kama askari wa makampuni ya ulinzi akiwa na kofia na mabuti.

Mkono mmoja alikuwa ameshika tochi iliyokuwa ikimmulika na mkono mwingine alishika sime ambayo tayari alikuwa ameipunga juu.

Alikuwa kama hatua kumi na tano hivi nyuma ya waziri.

Ule mwanga wa tochi sasa ulikuwa ukimpiga waziri usoni.

Kile kitendo cha kufumwa akiwa katika hatua ya kuutupa mwili huo kilimfanya ababaike na kutaharuki. Kadhalika ule mwanga wa tochi uliokuwa ukimmulika usoni ulimchanganya zaidi.

“Nimekuuliza wewe ni nani na unataka kufanya nini katika eneo hili?’ Mlinzi huyo alimuuliza tena waziri huku akikaza mwendo kumfuata.

Alikuwa amemkaribia sana.

Itaendelea kesho hapahapa tangakumekuchablog. 

KUMEKUCHA UPYA

No comments:

Post a Comment