Friday, September 23, 2016

MOROCCO YAOMBA KUJIUNGA NA AU

Morocco imewasilisha rasmi ombi la kutaka kujiunga upya na AU

Mzozo kuhusu Western Sahara umesababisha mgawanyiko kati ya Morocco na muungano wa Afrika
Muungano wa Afrika unasema Morocco imewasilisha rasmi ombi la kutaka kujiunga tena na muungano huo.
Morocco ilijitoa katika lililokuwa Shirika la Muungano wa Afrika OAU, zaidi ya miongo mitatu iliyopita kufuatia mzozo kuhusu eneo la Magharibi mwa Sahara
Muungano wa Afrika umelitambua eneo hilo kama taifa huru, wakati Morocco inalitazama kama sehemu ya eneo lake.
Muandishi wa BBC anasema inaonekana kuwa Morocco sasa inatambua kutokuwepo kwake kumepunguza ushawishi wake Afrika.
Inatarajia kuwa kwa kujiunga kwa mara nyengine na muungano wa Afrika itasaidia kuipa nafasi zaidi ya kushawishi mataifa mengine kuunga mkono msimamo wake kuhusu sehemu ya Magharibi mwa sahara
BBC

No comments:

Post a Comment