Friday, September 30, 2016

CHINA NA TEKONOLOJIA ZAKE, YAJENGA CHOO KWA VIOO

Vyoo vilivyojengwa kwa vioo vyazinduliwa nchini China

Mwanamume chooni Changsha, China, 29 Septemba 2016.Changsha, China, 29 Septemba 2016.Tianmen Mountain (1 Aug 2016)China imezidisha matumizi yake ya vioo kuunda vivutio vya kitalii kwa kujenga choo cha vioo ambacho mtu anaweza akaona nje na hata ndani.
Vyoo hivyo, vimejengwa karibu na Ziwa Shiyan, katika mkoa wa Hunan kusini mwa nchi hiyo.
Vioo hivyo vinawezesha wanaovitumia vyoo hivyo kutazama mandhari ya kuvutia ya msitu au wengine wanaotumia vyoo jirani.
Aidha, walio nje wanaweza kuona walio ndani ya vyoo
Kuta za vyoo hivyo, hata zile zinazotenganisha vyoo vya wanawake na wanaume, ni za vioo kabisa ingawa vioo hivyo vimetiwa ukungu kiasi.
Vyombo vya habari nchini humo vinasema ni watu wachache sana waliotumia vyoo hivyo siku ya kuzinduliwa kwake.

No comments:

Post a Comment