Wednesday, September 21, 2016

BABU NA MJKUU WAFIKI KWA KUUNGUA MOTO BAADA YA NYUMBA YAO KUUNGUA



Tangakumekuchablog
Tanga, MTOTO wa miaka 6  Mwanaisha Athumani na Balizahu Juma (50) wote wakazi  wa Manolo tarafa ya Mlalo Wilayani Lushoto Mkoani Tanga, wamefariki dunia na wengie wanne kujeruhiwa baada ya nyumba yao kuungua moto wakati wakiwa wamelala.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Leo, kamanda wa polisi Tanga, Benedickt Wakulyamba, alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 2; 30 usiku wakati wakijiandaa kulala.
Aliwataka majeruhi kuwa ni Rashid Juma (18), Omari Juma (15) na Hamad Juma (11) ambao wote wamelazwa katika hospitali ya Wilaya ya Lushoto kwa matibabu.
Alisema uchunguzi wa awali wa tukio hilo ni kibatari ambacho kiliripuka na kuwasha nguo ambazo zilikuwa karibu na kusambaa mpaka kwenye vitanda na kuunguza magodoro ya usufi.
“Mtoto wa miaka sita na mzee wa miaka hamsini wamekufa baada ya nyumba waliyokuwemo ndani kuungua yote kwa kushindwa kujinasua na moto ambao ulikuwa ukisambaa kwa kasi” alisema Wakulyamba na kuongeza
“Wakati wenzao wakijinasua kutoka katika nyumba ambavyo walikuwa wamelala wao chumba chao kilikuwa moto umeshauzingira kwani walikuwa chumba kimoja na chanzo ni kibatari ambacho kiliripuka na kuunguza nguo ambazo zilikuwa karibu” alisema
Katika tukuio jengine mkazi wa Chumbageni Tanga, Hamis Hamad (46) amefariki baada ya watu wasiojulikana kumshambuliwa kwa mawe na marungu kwa tuhuma za wizi.
Alisema kijana huyo ambaye alituhumiwa kuiba vifaa vya ndani ikiwemo Tv na Radio usiku wa saa 9 eneo la Chumbageni kwa kutumia baskeli na ndipo walinzi walipopiga kelele za mwizi.
‘Huyo kijana ni mwizi mzoefu na kw amuda mrefu polisi walikuwa wakimsaka kwa udi na uvumba kumsomea mashtaka na kumfikisha mahakamani na usiku wa kuamkia leo taarifa ni kuwa ameuwawa” alisema kamanda
Kamanda Wakulyamba amewataka wananchi kuacha kujichukulia sheria mikoni na badala yake watuhumiwa kuwafikisha polisi ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.
                                                            Mwisho

No comments:

Post a Comment