Saturday, October 29, 2016

POLISI WAZUIA KUFANYIIKA MKUTANO MAALUMU WA CUF TANGA


Tangakumekuchablog
Tanga, JESHI La Polisi Tanga limezuia kufanyika mkutano mkuu  maalumu wa Chama Cha Wananchi (CUF) Leo  ambao ungewajadili madiwani 12 ambao waliingia katika Baraza la Madiwani na  taarifa zilisema kuwa Katibu Mkuu, Maalimu Seif Sharif Hamad angekuwepo.
Taarifa za jeshi la polisi kwa vyombo vya habari zimedai kuwa  kuzuiwa kwa mkutano huo ni kitisho cha uvunjifu wa amani kutokana na kuwepo kwa makundi mawili yanayozozana.
Taarifa hiyo iliyotolewa na  Mkuu wa Polisi Wilaya ya Tanga, Idd Abdalla, zimeongeza kuwa ukumbi ambao mkutano huo ungelifanyika ni mdogo kutokana na wingi wa wanachama ikikumbukwa kuwa juma lililopita mkutano wa chama hicho ngazi ya Wilaya ulivunjika kwa vurugu.
Akizungujmza na waandishi wa habari,Mwenyekiti wa CUF Wilaya, Rashd Jumbe, alisema kuzuiwa kwa mkutano huo kutofanyika lengo la chama la kuwajadili madiwani hao upo pale pale.
Alisema kamati tendaji imependekeza madiwani 7 kati ya 12 kufukuzwa uanachama kutokana na kukiuka msimamo wa chama ambapo madiwani watano wako katika uchunguzi.
“Mkutano wetu polisi wameuzuia lakini niseme kuwa msimamo wa chama wa kuwafukuzwa wmadiwani waliokiuka msimamo watachukuliwa hatua na kufukuzwa” alisema Jumbe na kuonmgeza
“Katika fagio hili mbunge pia yumo kwani nae alishiriki kikamilifu pamoja na naibu meya, kwa sasa tunafanya utaratibu na jeshi la polisi kufuata vigezo wanavyotaka ili kuufanya mkutano huo tena” alisema
Akizungumzia uimara na mshikamano ndani ya chama, Jumbe alisema chama kiko imara na hakina mpasuko kama baadhi ya wapinzani wao wanavyodai hivyo kuwataka wanachama kufanya subra kipindi hiki cha kuwajadili madiwani waliokisaliti chama.
                                                    Mwisho

No comments:

Post a Comment