Monday, October 24, 2016

RIPOTI MAALUMU KWA WACHEZAJI MPIRA WA MIGUU

Utafiti umeonesha upigaji mpira kwa kichwa una madhara

mpira
Watafiti kutoka chuo kikuu cha Stirling huko Scotland wamegundua kuwa kumbukumbu ya mchezaji wa mpira wa miguu inaweza kuathirika kwa upigaji wa mpira kwa kutumia kichwa kwa muda mfupi.
Wanasema kuwa ufanyaji kazi wa kumbukumbu hupungua kwa kati ya asilimia 41 na 67 kulingana na idadi ya upigaji wa mpira  kwa kutumia kichwa na hurudi katika hali ya kawaida baada ya masaa 24.
Mmoja wa watafiti hao Dr Magdalena Letswaart amesema ingawa mabadiliko sio ya kudumu lakini kuna umuhimu katika Afya ya Ubongo, hivyo wachezaji wanatakiwa kuwa makini kwa upigaji huo  na  kinatokea ndani ya ubongo.
Chuo hicho kimesema kuwa watafanya uchunguzi ili kujua kama madhara yatakua ya kudumu baada ya kucheza mara kwa mara mpira wa miguu na kutumia kichwa.
BBC

No comments:

Post a Comment