Wednesday, July 29, 2015

AIRTEL YABORESHA HUDUMA ZAKE TANGA (YAZINDUA KITUO CHA KISASA CHA HUDUMA KWA WATEJA)


Tangakumekuchablog

Tanga, MKUU wa Mkoa wa Tanga, Said Magalulla, ameyataka makampuni ya simu nchini kupunguza gharama za matumizi ya simu ili kuwawezesha watu wa kipato cha chini kuweza kumudu matumizi ya mitandao hiyo.

Akizungumza mara baada ya kufungua kituo cha huduma kwa wateja cha kampuni ya simu ya Airtel mjini hapa  jana, Magalulla alisema gharama za matumizi ya simu ziko juu hivyo ni wajibu wa makampuni hayo nchini kumuangalia mtu wa kipato cha chini.

Alisema asilimia kubwa ya watumiaji wa simu   ni watu wa kipato cha chini jambo ambalo limekuwa kikwazo kwa maendeleo ya jamii na kuzidisha  ugumu wa maisha.

“Mawasiliano ya simu nchini yanazidi kukua kwa kasi ila changamoto iko katika gharama za matumizi-----tumeona gharama zikiongezeka lakini hatuoni zikipungua” alisema Magalula na kuongeza

“Hebu nyinyi airtel tuliopo hapa onyesheni mfano kwa wengine ili kuiga kutoka kwenu-----kufungua kituo kikubwa  cha huduma kwa wateja hapa kwetu ni wazi kuwa pato kubwa linatoka kwa mtumiaji tena wa kipato cha chini” alisema

Alisema kituo hicho kitakuwa msaada mkubwa kwa wananchi wa Tanga na watumiaji wa mtandao wa Airtel na hivyo kuitaka kuboresha huduma zake zikiwemo za watumiaji wa intareti  na simu.

Wakati huo huo  Mkurugenzi wa huduma kwa wateja Tanzania, Adriana Liamba, alisema malengo ya kampuni ya simu ya Airtel ni kumfikia kila mmoja wa mjini na vijijini na hivyo kuwa na mipango ya kupeleka huduma hiyo kila pembe.

Alisema mbali ya changamoto kampuni ya simu inayokumbana nayo lakini imeweza kusaidia jamii katika nyanja mbalimbali zikiwemo za kujenga majengo ya shule na zahanati pamoja na vifaa vya elimu kwa wanafunzi mashuleni.

“Kampuni inakabiliwa na changamoto mbalimbali kuhakikisha kila mtu inamfikia huduma ya mtandao katika eneo alilo----ikumbukwe kuwa tumefanya mengi mazuri yakiwemo kujenga majengo ya shule na vituo vya afya” alisema Liamba

Ameitaka jamii kushirikiana na kampuni ya Airtel ili kuweza kurahisha maendeleo na ustawi wa uchumi wa nchi na kila mmoja kufaidika na huduma hiyo muhimu kwa jamii.

                                                    Mwisho

 Mkurugenzi wa huduma kwa wateja  kampuni ya simu ya Airtel Tanzania, Adriana Liamba, akizungumza wakati wa ufunguzi wa kituo kipya  cha huduma kwa wateja kilichopo jengo la Nyumbani Hotel Tanga juzi. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Said Magalulla.
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Said Magalulla, akikata uzi kufungua kituo kipya  cha huduma kwa wateja kampuni ya simu ya Airtel kilichopo jengo la Nyumbani Hotel Tanga juzi. Kushoto ni Mkurugenzi wa huduma kwa wateja Tanzania  kampuni ya simu ya Airtel, Adriana Liamba.

 Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Said Magalula akiangalia aina za simu ndani ya kituo kipya cha  huduma kwa wateja kampuni ya simu ya Airtel iliyopo ndani ya jengo la Nyumbani Hotel. Kilia anaetoa maelekezo ni mkurugenzi mkuu huduma kwa wateja kampuni ya simu ya Airtel Tanzania, Adriana Liamba.

 Mkurugenzi wa huduma kwa wateja Tanzania, kampuni ya simu ya Airtel, Adriana Liamba, akitoa  maelekezo ya shughuli zao kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Said Magalulla ndani ya kituo kipya cha huduma kwa wateja cha kampuni hiyo kilichozinduliwa juzi Tanga.


No comments:

Post a Comment