Friday, July 31, 2015

WAKALI KUPEPETANA WEMBLEY

Ngao ya Jamii Ligi Kuu England ni Chelsea Vs Arsenal Jumapili hii,wengine je?..

ligi
Kipenga cha kuanza kwa ligi kuu ya England msimu mpya kinatarajia kupulizwa jumapili hii wakati mabingwa Chelsea watakapovaana na Arsenal katika mchezo wa ngao ya jamii.
Mchezo huo utapigwa katika uwanja wa Wembley,London.
Ligi kuu ya Uingereza inatarajia kuanza Agosti 8 kwa michezo sita ambapo Manchester United vs Tottenham katika uwanja wao wa nyumbani wa Old Trafford wakati Bournemouth vs Aston Villa, Norwich city vs Crystal palace ,Everton vs Watford na Chelsea vs Swansea city.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment