Friday, July 31, 2015

UZINDUZI JEZI MPYA YA SIMBA NA MADUKA YAKE LEO

Club ya Simba SC kwenye headlines moja na Real Madrid, Barca na Manchester United.

BarcelonaKila mwaka klabu ya Simba huwa na utamaduni wa kufanya tamasha la kutambulisha jezi, wachezaji na mipango mingine ya klabu hiyo.Tamasha hilo linalojulikana kama Simba Day  kwa mwaka huu haitakuwa Simba Day bali ni wiki ya Simba. Mabadiliko hayo yametokana na maboresho kadhaa ambayo yamefanywa na uongozi.
Haji-Manara-SimbaUzinduzi huo utafanyika siku ya Jumamosi  August 1 katikati ya jiji la Dar Es Salaam saa 4:30, kwa mujibu wa mkuu wa idara ya habari ya Simba, Haji Manara amethibitisha kufanyika kwa mambo mbalimbali ikiwemo uzinduzi wa maduka yatakayouza jezi za Simba, mabegi, kalamu, kofia na vitu vingine mbalimbali vyenye logo ya Simba ikiwa ni sehemu nyingine ya kuuongeza uchumi wa club.
Kikosi cha SimbaManara amethibitisha kuwepo kwa maduka ya bidhaa za klabu sehemu mbalimbali ikiwemo Mlimani City, huku kilele cha Wiki ya Simba itakuwa August 8 Uwanja wa Taifa Dar Es Salaam kwa Simba kucheza mchezo wa kirafiki na klabu ya FC Leopard ya Kenya. Hata hivyo Manara amekanusha madai yanayosambaa kuwa mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi Laudit Mavugo hatokuja Simba.
Simba-Sports-Club“Mavugo nimeona kwenye gazeti nimesikitishwa sana, wiki iliyokwisha gazeti hilohilo liliandika Okwi anarejea Msimbazi hata chezea tena klabu yake ya Denmark wakaandika bila kuweka source bila kubalance story nawahakikishia Mavugo siku ya tarehe 8 August atacheza mechi ya Simba day “>>> Haji Manara
simba-sports-club-dylan-kerr1Ungana nami kwa habari motomoto za papo kwa papo , ni ha hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment