Monday, July 27, 2015

MANCHESTER UNITED YAZIDI KUKIMARISHA KIKOSI CHAKE

Good News kwa Manchester United na kipa huyu kutoka Argentina….

van gaal
Wakati klabu mbali zikiendelea na zoezi la kuandaa timu zao kwa ajili ya msimu mpya wa ligi kuu, tayari Manchester United imemsainisha kipa wa Argentina, Sergio Romero kwa mkataba wa miaka mitatu.
Kipa huyo  anachukua nafasi ya mkongwe Victor Valdes aliyekosana na Kocha wake Luois van Gaal.
Romero aliwahi kufanya kazi akiwa anafundishwa na van Gaal wakati wakiwa katika klabu ya AZ Alkmaar mwaka 2009.
Kipa huyo mwenye uwezo wa juu  ataongeza ushindani na David De Gea ambaye imekuwa ikielezwa anataka kujiunga na Real Madrid.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment