Thursday, July 30, 2015

CHEMCHEM ILIYOSAHAULIKA KIJIJI CHA MAJIMOTO AMBONI ,TANGA


Tangakumekuchablog

Tanga, WAKAZI wa kijiji cha Majimoto kata ya Mafuriko halmashauri ya jiji la Tanga, wameshangazwa na Wizara ya Utalii na Maliasili kuacha kuifanya  chemchem inayotoa maji  moto iliyoko kijiji hapo kuwa ya kitalii  hatua ambayo inaikosesha Serikali mapato.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, wakazi hao walisema Chemchem hiyo imekuwa kivutio jambo ambalo wageni kutoka mataifa ya nje hufika na kujionea maajabu ilhali Serikali imeshindwa kuitambua.

Alisema kutokana na kutokuwepo kwa utaratibu wageni wa nje na ndani hufika bila kizuizi na kujionea maajabu ya Chemchem hiyo ambayo hutoa maji ya moto pamoja na maajabu mengine yaliyopo eneo hilo.

“Serikali inatambua uwepo wa chemchem hii inayotoa maji moto si usiku wala mchana na haina kiangazi wala masika----raia wa kigeni wanaitambua ila sisi hatuna habari nayo” alisema Hamad Pinto na kuongeza

“Kama Serikali ingeweka utaratibu wa kukiweka kituo hiki katika mazingira ya utalii ingeweza kuongeza mapato yake-----watu wanakuja  bila mpangilio na kupiga picha na kushangaa shangaa” alisema

Kwa upande wake mkazi wa Amboni, Mussa Juma, alisema kuna vivutio vingi vya utalii eneo hilo lakini havitambuliki yakiwemo majengo ya kale na misitu yenye wanyama.

Alisema kama Serikali ingeliviendeleza vivutio hivyo na vijana  kupata ajira na kuondokana na ukaaji wa vijiweni jambo ambalo linawasukuma kujitumbukiza katika viwashawishi.

Alisema vijana wengi hawana kazi na wamekuwa wakikaa vijiweni hivyo kuwepo kwa vivutio hivyo na kuendelezwa ingweza kupunguza wimbi la umasikini na ajira kwa vijana.

“Vinaja wengi hawana ajira wala kazi ya kujiajiri na badala yake wamekuwa wakikaa vijiweni kupiga soga-----kama vivutio vya kitalii vipo kuna sababu gani ya kuacha kuendelezwa” alisema Juma

Alisema ili kuweza kupunguza umasikini ni vyema Serikali kuviendeleza vivutio vyake jambo ambalo linaweza kuingiza mapato na kuweza kupunguza umasikini majumbani.
                                                        Mwisho

 Mkazi wa kijiji cha Majimoto kata ya Amboni Tanga, Hamad Pinto akiwaonyesha waandishi wa habari  maji ya moto katika chemchem iliyopo eneo la Kidugaro  inayotoa maji moto. Chemchem hiyo inadaiwa kuwepo toka mwaka 1935,




No comments:

Post a Comment