Monday, July 27, 2015

PANGANI WALIA NA UKUTA MTO PANGANI

Tangakumekuchablog

Pangani, WAKAZI wa Pangani Wilayani hapa wameikumbusha Serikali  kuujenga ukuta wa mto Pangani ulioanguka ili kuepusha kitisho cha  maji kuingia mitaani nyakati za upepo na mvua.

Wakizungumza na waandishi wa habari jana, wakazi hao walisema hadi za sasa hakuna dalili zozote za matumaini ya kuanza ujengwaji wa ukuta huo jambo ambalo limekuwa likiwapa  hofu nyakati za mvua na upepo.

Walisema kwa kipindi kirefu viongozi wa Serikali wamekuwa wakitoa ahadi ya kujengwa kwa ukuta huo ulioanguka na kudai kuwa yapata zaidi ya  miaka saba na hivyo matumaini hayo kufifia.

“Tunashukuru nyinyi waandishi kuja kujionea hatari ya maji kuingia mitaani----ukuta huu umekuwa ukitolewa ahadi na viongozi mbalimbali wa Serikali na vyama na leo uoneni hali ilivyo” alisema Said Khamis na kuongeza

“Kuelekea uchaguzi mkuu tunawaomba waomba kura kuliweka katika ahadi zai zao huu  ukuta kwani hali inazidi kuwa mbaya kila siku ziendavyo kwani maji yapasua njia kuelekea mitaani” alisema

Wakati huo huo mkazi wa Mkwaja, Ali Mikidadi, ameitaka Wakala wa ufundi na Umeme  kuongea kivuko chengine badala ya cha sasa kimoja kinachotoa huduma na kuwa kero.

Alisema wafanyabiasha na wafanyakazi wamekuwa wakichelewa kufika katika maeneo yao ya kazi kutokana na kivuko kuwa kimoja na hivyo kuchukua muda mrefu kuweza kuvuka kwa wakati.

“Kwa muda mrefu ni kivuko kimoja tu ndicho kinachotoa huduma na kuwa kero kwa wafanyakazi wa wafanyabiashara----- wafanyabiashara wa mbogamboga na matunda  hufika masokoni muda kuchelewa na kukuta wanunuzi wameshaondoka” alisema Mikidadi

Alisema ili kuweza kuondosha kero kwa wakazi wa pande mbili hizo ni vyema Tamesa inayosimamia kivuko hicho kuweka kivuko cha pili ili kuondosha kero kwa wakazi wa Pangani na maeneo mengine.

                                                  Mwisho


No comments:

Post a Comment