Friday, July 24, 2015

VIBOPA WA ARSENAL WAMTAKA WENGER KUVUNJA SANDUKU LA PESA

Mkurugenzi wa Arsenal anataka Wenger avunje rekodi ya usajili? Wana pesa? Cheki walivyojipanga..

ddfd8772d2ae484b79556a5a46a1d42a_XL
Klabu ya Arsenal ya Uingereza miaka kadhaa nyuma ilikuwa ni nadra sana kukuta inasajili mchezaji kwa gharama za juu ila kufuatia falsafa za kocha Arsene Wenger ambae anaaminika kuwa hakutaka kukubali kuwa soka limebadilika na wachezaji wananunuliwa kwa gharama za juu, yeye alikuwa akiendelea kuwatumia wachezaji makinda na kununua wachezaji kwa gharama nafuu.
Arsenal's French manager Arsene Wenger gestures to the fans during the English Premier League football match between Newcastle United and Arsenal at St James' Park in Newcastle Upon Tyne, northeast England, on May 19, 2013.  AFP PHOTO / IAN MACNICOL RESTRICTED TO EDITORIAL USE. No use with unauthorized audio, video, data, fixture lists, club/league logos or ?live? services. Online in-match use limited to 45 images, no video emulation. No use in betting, games or single club/league/player publications.        (Photo credit should read Ian MacNicol/AFP/Getty Images)
Wenger alionekana kuanza kukubali kwamba soka limebadilika baada ya kuwasajili Mesut Ozil kutokea Real Madrid kwa ada ya uhamisho wa pound milioni 42 mwaka 2013 na kumsajili Alexis Sanchez kwa ada ya uhamisho wa pound milioni 35 akitokea FC Barcelona.
gun__1378990173_Ozil
Kufuatia mpango wa kuboresha kikosi hicho cha Emirates mkurugenzi wa Arsenal Lord Harris amethibitisha kuwa Arsene Wenger ana uwezo wa kumsajili mchezaji yoyote duniani kwa sasa.
Licha ya Wenger kukubali kuwa Arsenal kwa miaka ya hivi karibuni imekuwa ikishindwa kutwaa taji la Ligi Kuu Uingereza ila Lord Harris amethibitisha Arsenal kuwa imetenga bajeti ya pound milioni 200 kwa ajili ya kuimarisha kikosi chao.
Arsenal Training Session
Arsene Wenger anaweza kumnunua mchezaji yoyote duniani, suala la fedha lilikuwa gumu kwetu wakati tunahamia Emirates lakini sasa tuko huru… katika account ya benki tuna pound milioni 200. Hakuna mpango wa kumsajili mchezaji yoyote isipokuwa kama atapata mchezaji nyota kama Ozil au Sanchez, lakini anaangalia mmoja kati ya wachezaji ambao hawapatikani”>>> Lord Harris
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment