Sunday, February 28, 2016

MAJI MAREFU ASAIDIA VILABU VYA MICHEZO KOROGWE VIFAA MILIONI 5



Tangakumekuchablog
Korogwe, MBUNGE wa jimbo la Korogwe Vijijini, Stivin Ngonyani, maarufu kama Profesa Majimarefu, ametoa jezi seti tano, mipira mitatu vyenye thamani zaidi ya shilingi laki 5 kwa timu ya mpira ya vijana wa Makuyuni Wilayani Korogwe lengo likiwa ni kukuza vipaji.
Vifaa hivyo kwa mujibu wa Mbunge huyo vimekuja kufuatia maombi ya vijana wa Makuyuni kumtaka kusaidia ili kuweza kuimarisha timu yao na kuingia ligi ngazi ya Wilaya hadi Mkoa.
Alisema msaada huo hautoishia hapo lakini atapenda kuona timu hiyo inafanya vizuri ligi ngazi ya Tarafa na kuahidi kuisaidia kwa hali na mali hivyo kuwataka kuonyesha moyo na mapenzi na timu.
“Leo nawapeni jezi na mipira kumaliza kilio chenu kwani nakumbuka barua yenu muloniandikia nikiwa bungeni na mukaiacha kwa katibu wangu pale ofisini, niwaahidi kuwa mimi kama mbunge wenu nitakuwa nanyi bega kwa bega” alisema Majimarefu na kuongeza
“Nitahakikisha timu yenu inaingia mashindano ya Wilaya hadi mkoa na mimi kuwa mlezi wenu na musisite kunieleza kwa lolote” alisema
Kwa upande wake Kocha wa timu hiyo, Mbaraka Kiondo, alimshukuru mbunge huyo na kusema kuwa msaada wake huo aloutoa utatumika kama ilivyo na kumuahidi kuwa hawatamuangusha katika mashindano ya ligi.
Alisema awali walikuwa wanatumia mipra mmoja huku wakiwa hawana jezi na badala yake kila mchezaji alikuwa anatumia fulana yake jambo ambalo lilikuwa kero wakati wa uchezaji na kutoelewana.
“Mheshimiwa Mbunge hatuna la kukulipa na hatuna la kusema kwani hatujui tuanze wapi ila nimalize kwa kusema asante sana na Mungu ndie atakakulipa na kukubariki” alisema Kiondo
Aliwataka wachezaji wake kuzingatia muda wa kufanya mazoezi baada ya kupata vifaa hivyo na kuwataka kupiga kambi ili kushikilia usukani wa ligi hiyo ngazi ya Tarafa na msimu wa ligi kuingia ngazi ya Wilaya.
                                                Mwisho

No comments:

Post a Comment