Friday, February 5, 2016

OZIL WA ARSENAL AVUTWA SHATI

Mesut Ozil sio tena mfalme wa assist, huyu ndio jamaa aliyechukua nafasi yake …

Wiki kadhaa nyuma kiungo wa kimataifa wa Ujerumani anayeichezea klabu ya Arsenal ya Uingereza Mesut Ozil alikuwa anatajwa kama assist King, ikiwa na maanakuwa yeye ndio mtaalam wa assist au mkali wa assist, lakini February 4 stori kutoka sokkaa.com inaripoti kuwa amezidiwa na kuwa nafasi ya pili sawa na Neymar wa klabu ya FC Barcelona. Hii ndio TOP 6 ya wachezaji wanaoongoza kwa assists.
6-Luis Suarez- Mshambuliaji wa kimataifa wa Uruguay anayeichezea klabu ya FC Barcelona ya Hispania ambaye usiku wa kuamkia February 4 alifunga goli nne dhidi ya Valencia na kufikisha jumla ya magoli 35 katika michezo 33, Suarez yupo nafasi ya sita kwa kutoa jumla ya assist 11.
Luis Suarez
5- Angel Di Maria- Huenda klabu ya Man United na mashabiki wake hawafurahii hili kutokana na mchezaji huyo kahama klabu yao, Di Maria anatajwa kufanya vizuri ndani ya klabu ya Paris Saint Germain ya Ufaransa. PSG hadi sasa hawajapoteza mchezo wowote msimu huu, lakini good news nyingine ni kuwa Di Maria ana jumla ya assist 12 na magoli 12.
epa05009775 Paris Saint-Germain's Argentinian Angel Di Maria (R) vies for the ball with Real Madrid's Isco during the UEFA Champions League group A soccer match between Real Madrid and Paris Saint-Germain (PSG) at Santiago Bernabeu stadium, in Madrid, Spain, 03 November 2015.  EPA/JUANJO MARTIN
epa05009775 Paris Saint-Germain’s Argentinian Angel Di Maria (R) vies for the ball with Real Madrid’s Isco during the UEFA Champions League group A soccer match between Real Madrid and Paris Saint-Germain (PSG) at Santiago Bernabeu stadium, in Madrid, Spain, 03 November 2015. EPA/JUANJO MARTIN
4- Kevin De Bruyne kutoka klabu ya Man City na timu ya taifa ya Ubelgijia, amekuwa na mchango mkubwa msimu huu ndani ya klabu ya Man City msimu huu, licha ya kuwa ana assist sawa na Di Maria, De Bruyne amewekwa nafasi ya nne.
the Barclays Premier League match between Manchester City and Newcastle United at Etihad Stadium on October 3, 2015 in Manchester, United Kingdom.
the Barclays Premier League match between Manchester City and Newcastle United at Etihad Stadium on October 3, 2015 in Manchester, United Kingdom.
3- Mesut Ozil- ndio alikuwa kinara wa kutoa assist nyingi katika mechi moja, kwani aliweka rekodi ya kutoa assist zaidi ya moja katika mechi nne mfululizo, Ozil kwa sasa bado ana assist 16 sawa na Neymar.
Ozil-injured1-700x453
2- Neymar- amekuwa nafasi ya pili kwa kuwa na jumla ya assist 16 sawa na Ozil ila yeye kafunga jumla ya goli 21, katika mechi 28 za mashindano yote.
Neymar111
1- Henrikh Mkhitaryan wa Borussia Dortmund kwa sasa ndio unaweza muita assist king kwa bara la Ulaya, ana jumla ya assist 17 na goli 17,  hizo ni assist za jumla ya mashindano yote aliyocheza hadi sasa msimu huu.
Henrikh-Mkhitaryan2
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa Tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment