Tuesday, February 23, 2016

WACHAMBUZI WA SOKA WAIPA UJANJA ARSENAL KUIMALIZA BARCELONA



Wachambuzi wa masuala ya soka nchini England, wameishauri Arsenal kushambulia huku ikimpa kashkash kiungo Sergio Bosquet ili iishinde Barcelona.

Ushauri huo umeendana na kuitaka Arsenal kuachana na kujilinda muda mwingi ikiwa katika lango lake kwa kuwa ni kazi kuwadhibiti washambuliaji watatu hatari wa Barcelona, Lionel Messi, Neymar na Luis Suarez.

Arsenal itakuwa uwanjani LEO  kuwavaa Barcelona katika mechi ya Ligi ya Mabingwa inayotarajia kutazamwa na mashabiki wengi zaidi kuliko nyingine zote.


Barcelona inaonekana kuwa mwiba kwa kila timu kipindi hiki na inaonekana kuwa timu isiyofungika.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa Tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment