Friday, February 19, 2016

NDANI YA MASAA 20 WAZIRI MKUU KUTUMBUA JIPU BANDARI YA TANGA (TPA)



Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akitembelea bandari ya Tanga (TPA) Leo  wakati wa ziara ya kushtukiza na kuagiza kupatiwa maelezo ya ununuzi wa matishali matatu ambayo hayana uwezo  badala ya mawili yaliyoidhinishwa na Serikali na kutaka ndani ya masaa 20 taarifa hiyo iwe imeshafika ofisni kwake.
Majaliwa ambaye ametua Tanga kwa kushtukiza na kwenda bandari ya Tanga moja kwa moja kujionea mambo yaendavyo pia alitoa agizo kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mwantumu Mahiza pamoja na jeshi la Polisi kuongeza doria katika mwambao wa Bahari ya Hindi kuzuia mali za magendo pamoja na uingizaji wa Sukari kutoka nje ambayo imepigwa marufuku.
Alisema Mwambao wa Bahari ya Hindi upande wa Tanga ni kinara wa uingizaji wa mali za magendo hivyo kutaka kikomeshwa mara moja shughuli hizo na kuongeza kikosi kazi ya kupambana na mali za magendo










 Injinia wa Mamlaka Bandari Tanzania (TPA), Felex Mafinga, akitoa maelekezo kwa Waziri Mkuu Kassim Mjaliwa  juu ya ununuzi wa matishali matatu ambayo hayana uwezo  badala ya mawili yaliyoidhinishwa na Serikali hivyo kuagiza kupatiwa maelezo ndani ya masaa 20 iwe imeshafika ofisini kwake.




No comments:

Post a Comment