Saturday, February 13, 2016

MBUNGE WA MLALO AWATA WAKULIMA WA MBOGAMBOGA KULICHANGAMKIA SOKO LA PAMOJA



Tangakumekuchablog
Mlalo, MBUNGE wa jimbo la Mlalo, Rashid Shangazi,(CCM) amewataka wakulima wa mbogamboga na matunda Wilayani Lushoto kulichangamkia soko la pamoja la Afrika Mashariki na kuacha kusubiri walanguzi wa mazao yao mashambani.
Akizungumza  na wakulima wa Mlalo, Bumbuli  na Lushoto jana wakati wa kikao cha wadau wa kilimo cha mbogamboga na matunda, Shangazi alisema wakulima wengi hawana taarifa la soko la pamoja hivyo kutakiwa kuelimishwa.
Alisema ni wakulima wachache ambao wako na uelewa wa soko hilona wengi wao wakiwa hawana uelewa ambalo kwa miaka mingi wamekuwa mtaji wa matajiri na kurudisha nyuma sekta ya kilimo cha mbogamboga na matunda Wilayani humo.
“Kuna soko la pamoja ambalo limefunguliwa zamani tu, nashangaa sioni mkulima hata mmoja hapa anaepeleka mazao yake moja katika soko linalounda umoja huo zaidi ya wenzetu tu” alisema Shangazi na kuongeza
“Nchi zetu moja ya malengo yake ni hizi za kuwasaidia wakulima na wajasiriamali kutangaza kazi zao na kuuza katika masoko na kuweza kuongeza kipato cha kazi zao pamoja na kujifunza” alisema
Shangazi alisema ofisi yake ya  Ubunge imejipanga kuhakikisha mkulima wa mboga mboga na matunda anayafikia masoko ili kuweza kujinasua na ukiritimba wa kulanguliwa bei na wafanyabiashara wenye pesa.
Kwa upande wake mkulima wa nyanya na maboga, Shembilu Saleh, alisema wakulima wengi wanakabiliwa na changamoto ya kuweza kuwakabili  wadudu waharibifu wa mazao baada ya gharama za madawa kuwa bei ya juu.
Alisema ni vyema Serikali kupunguza gharama za uagiziaji wa madawa ya wadudu wa mbogamboga na matunda kwani wengi wao wamekuwa wakishindwa kumudu na badala yake hulima kilimo cha kubahatisha.
Alisema wakulima wengi ni wakulima wa kipato cha chini ambao hulima kwa jembe la mkono hivyo  kushindwa kumudu gharama za kununua madawa na mbolea ya mimea yao.
“Sisi wakulima wadogo wa jembe la mkono hatuna mabadiliko kila misimu ya mavuno, kwanza tuko na changamoto za madawa ya wadudu kwani gharama ziko juu” alisema Saleh
Ameiomba Serikali kuwaokoa wakulima wadogowadogo kwa kuwawezesha kupata dawa za wadudu kwa gharama nafuu ili kuweza kufikia malengo yao na kuwa wakulima wa kisasa na kuachana na kilimo cha jembe.
                                               Mwisho

No comments:

Post a Comment