Sunday, February 7, 2016

SHULE IKO NA WALIMU WATATU WANAFUNZI 33



Tangakumekuchablog
Korogwe, SHULE ya msingi Mbuyuni kijiji cha Toronto Tarafa ya Mombo Wilayani Korogwe Mkoani Tanga, iko na walimu watatu na wanafunzi 33 baada ya  wanafunzi wengi ambao ni watoto wa wafugaji jamii ya kimasai kuyakimbia maeneo yao kutokana na migogoro ya ardhi.
Akizungumza na waandishi wa habari  Mwenyekiti wa kitongoji, Mathayo Sangula, alisema shule hiyo wanafunzi  wengi wanaosoma shuleni hapo  ni jamii ya wafugaji.
Amesema kutokana na mgogoro wa ardhi unaoendelea wafugaji wengi wameyahama  maeneo yao  hivyo shule hiyo  kubakiwa na walimu watatu na wanafunzi 33 na darasa la tatu kufutwa  baada ya kukosa wanafunzi darasani.
Alisema darasa la saba  liko na wanafunzi watatu ambao wanatarajiwa kufanya mitihani yao ya taifa ya kuingia kidato cha pili wanakabiliwa na changamoto kubwa  ya kuhakikisha wanamaliza silabasi zote kabla ya mitihani.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa kamati ya shule, Rajab Hassan, ameitaka Serikali kuinusuru shule hiyo kwa kuondosha utengamano baina ya wafugaji na wakulima pamoja na wawekezaji.
Amesema shule hiyo iko na kero nyingi ikiwemo  maji na matundu ya vyoo jambo ambalo limechangia kwa baadhi ya walimu kuacha kufundisha shuleni hapo.
                                           Mwisho






 Vijana wa Kimasai wakipita shule ya msingi ya Mbuyuni ambayo iko na walimu watatu na wanafunzi 33


No comments:

Post a Comment