Monday, May 23, 2016

BIASHARA BARABARANI


Wafanyabiashara maarufu kama Wamachinga barabara ya Morogoro Road Ubungo Dar es Salaam, wakitafuta wateja wa bidhaa zao kupitia madirisha ya magari Leo kama walivyokutwa na mpiga picha wa tangakumekuchablog
Utafutaji wa wateja kupitia madirisha ya vioo vya mabasi na magari ya kawaida yamekuwa yakigharimu wauzaji na wateja kwa namna tofauti.
Wateja wamekuwa wakidhulumiwa pesa zao mara baada ya kutoa pesa baada ya muuzaji kukimbia na kuwa ngumu kuacha gari na kumfuata kusikojulikana.
Kwa upande wa wafanyabiashara wao ni aghlabu kudhulumiwa au kufanyiwa utapeli kwani ni jambo ambalo wanalijua na kwanza hutaka mtu kutanguliza pesa.
Ni vyema unapotembelea miji mikubwa yenya foleni ya magari kama Dar es Salaam kuwa na tahadhari na vitu kama hivyo.




No comments:

Post a Comment