Sunday, May 22, 2016

MOURINHO KUWA BOSI MPYA WA MAN U

Mourinho kuteuliwa meneja wa Man U

Klabu ya Manchester United kinatarajiwa kumteua Jose Mourinho kama meneja wao mpya.
Inaaminika kuwa mkataba na Mourinho, raia wa Ureno mwenye umri wa miaka 53 uliafikiwa kabla ya mechi ya fainali kati ya Crystal Palace na Man U, ambapo Man U ilishinda kwa mabao 2-1.
Kufuatia kushindwa kwa Manchester United kufuzu kwa mechi za Champions League chini ya ukufunzi wa Louis van Gaal. ilkuwa bayana kuwa usimamizi ulihitaji kufanyiwa mabadiliko.
Mourinho amekuwa bila kazi tangu afutwe na klabu ya Chelsea mwezi Desemba.
Manchester United inapanga kuwasilia kwake wiki ijayo, baada ya kumfahamisha Van Gaal kuwa muda wake umekwisha.

No comments:

Post a Comment