Sunday, May 29, 2016

MAONYESHO YA BIASHARA TANTRADE YAFUNGULIWA TANGA LEO

 WATUMISHI wa Halmashauri ya jiji la Tanga wakibadilishana mawazo na wafanyakazi wa Shirika la Utangazaji la TBC wakati wa maonyesho ya nne ya Tan Trade yanayofanyika kwa siku 10 Mwahako nje kidogo ya jiji la Tanga

 Mwandishi wa Shirika la Utangazaji TBC Mkoani Tanga, Betha Mwambellah, akiangalia moja ya bidhaa katika maonyesho ya Kibiashara yanayofanyika Tanga ambayo yamefunguliwa na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Chales Mwaijage leo.
 Waandishi wa habari Mkoani Tanga, Tunu Ligombe wa Cluud TV  (kulia) na Betha Mwambellah wa Shirika la Utangazaji (TBC) wakishangaa moja ya bidhaa za maonyesho yaliyofunguliwa leo Tanga.


 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Chales Mwijage, akikata utepe kuzindua  maonyesho ya nne ya biashara (Tan Trade) yanayofanyika Mwahako nje kidogo ya jiji la Tanga yanayofanyika kwa siku kumi .



 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Chales Mwijage, akipokea zawadi iliyotolewa na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Tanga na Kaimu Meneja wa Bandari Tanga, Tryphone Ntipi  wakati wa maonyesho ya biashara (Tan Trade) yaliyofunguliwa leo Mwahako nje kidogo ya jiji la Tanga yanayofanyika kwa siku 10.
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Chales Mwijage akipata Qahwa wakati wa maonyesho ya Biashara aliyoyazindua leo Tanga
  Waziri wa Viwanda, Biashara na Uchukuzi, Chales Mwijage, akiangalia viatu katika moja ya mabanda ya maonyesho ya biashara (Tan Trade) yanayofanyika Mwahako nje kidogo ya jiji la Tanga maonyesho ambayo yanafanyika kwa siku 10 na kufunguliwa leo.



Mwandishi wa Shirika la Utangazaji (TBC) Betha Mwambellah akifurahia jambo wakati wa maonyesho ya nne ya Tantrade yaliyofunguliwa leo na Waziri wa Biashara, Viwanda na Uwekezaji, Chales Mwijage.

No comments:

Post a Comment