Friday, May 20, 2016

SAA YA HAILE SELASSIE ILIYOIBWA WAKATI WA MAPINDUZI YAPATIKANA

Saa ya Haile Selassie yarejeshewa ‘mmiliki’

Maafisa wa mahakama nchini Uswizi wameamua kukabidhi saa iliyotumiwa na Mfalme Haile Selassie kwa mtu aliyepatikana na saa hiyo, shirika la habari la Bloomberg limeripoti.
Familia ya Selassie ilisema saa hiyo iliibiwa kutoka kwenye Kasri la Mfalme na wanajeshi waliotekeleza mapinduzi ya serikali mwaka 1974 au ikaibiwa kutoka kwenye sefu muda mfupi baada ya mapinduzi.
Bloomberg wanasema saa hiyo ya muundo wa Patek Phillipe iliyopambwa kwa dhahabu inaweza kuuzwa £1m (£690,000) kwenye mnada.
Kampuni ya kupiga mnada ya Christie imekataa kufichua jina la mtu anayemiliki saa hiyo na ambaye anapanga kuiuza mnadani.

No comments:

Post a Comment