Sunday, April 23, 2017

MCHUNGAJI WA KANISA ATAKA AMANI IENZIWE



Tanga, MCHUNGAJI Kanisa la Sabato Centrol Tanga, Jackson Mdingi, ameitaka jamii kudumisha upendo na mshikamano pamoja na kuwa na huruma watu wasiojiweza.
Akizungumza mara baada ya kufanya usafi wa mazingira kwa ushirikiano na jeshi la polisi kutoka ofisi ya kamanda wa polisi pamoja na viongozi wa dini jana, Mdingi alisema amani iliyipo inafaa kuenziwa.
Alisema jamii inatakuwa kulikumbuka kundi la watu wasiojiweza kwa kuwapa misaada mbalimbali ikiwemo vyakula na kufanya usafi katika maeneo yao.
“Hapa tupo makundi mbalimbali yakiwemo viongozi wa dini na maofisa wa polisi pamoja na wawakilishi wa madhehebu ya dini, huu ni udhihirisho kuwa tuko wamoja hivyo tuuenzi” alisema Mdingi
Aliwataka viongozi wa dini kuwa na ada ya kuandaa matamasha na makongamano  ambayo yatashirikisha makundi mbalimbali ya dini jambo ambalo litawawezesha kubadilisha mawazo na kudumisha umoja.
Kwa upande wake, Kamanda wa polisi Mkoani Tanga, Benedickti Wakulyamba, alisema jeshi hilo litahakikisha linalinda watu na mali zao pamoja na kuendeleza msako wa wauzaji wa mihadarati ikiwemo mirungi.
Alisema wameunda kikosi maalumu ya kupambana na wapitishaji wa madawa ya kulevya na mali za magendo katika njia za panya zikiwemo za baharini.
“Jeshi la polisi liko makini na tumefanikiwa kuzuia mianya ya upitishaji wa madawa ya kulevya ikiwemo mirungi, kwa sasa tunafanya msako wa watumiaji kwa kuwafuata wanakokula” alisema Wakulyamba
Nae Diwani wa kata ya Mzizima, Fredick Chales amezitaka taasisi nyengine za dini kuiga mfano wa kanisa la Sabato  kwa kufanya kazi za kijamii kwa pamoja.
Alisema kufanya hivyo itasaidia kuleta mshikamano na umoja na kuondosha matabaka ambayo yanayoweza kuwagawa wananchi jambo ambalo halitakikani kutokea.





Maofisa Afya jiji wakijimuika na wakazi wa jiji la Tanga kufanya usafi wa mazingira kijijic ha miaka 21 .

No comments:

Post a Comment