Sunday, April 30, 2017

SUNDERLAND YASHUKA DARAJA, DEFOE KUCHEZA MCHANGANI

Mshambuliaji wa Sunderland Jermain DefoeKipindi cha miaka kumi cha klabu ya Sunderland katika ligi ya Uingereza hatimaye kimekwisha baada ya kushindwa na Bournemouth nyumbani.
Matokeo hayo pamoja na yale ya sare kati ya Hull City na Southampton yanamaanisha timu hiyo ya David Moyes ina pointi 14 ikiwa imesalia mechi nne.
Joshua King wa Bournemouth alifunga bao la pekee ikiwa imesalia dakika 2 na kuipa ushindi timu yake.
Raia huyo wa Norway pia karibu afunge katika dakika ya 20 lakini shambulio lake lilipiga mwamba wa goli na kurudi katika mikono ya kipa Pickford.
Hiyo ni mara ya 23 ya Sunderland kupoteza ,hatua inayomaanisha timu hiyo ya Black Cat imeshushwa dajara kutoka ligi ya Uingereza kwa mara ya nne.

No comments:

Post a Comment