Saturday, April 22, 2017

SIMULIZI, NILIKIONA CHA ,OTO URITHI WA BABU SEHEMU YA 13

ZULIA LA FAKI
 
NILIKIONA CHA MTO URITHI WA  BABU 13
 
ILIPOISHIA
 
Kama vile magoti yalimnyong’onyea, mzee alirudi ghafla kwenye kiti chake.
 
“Kwanini ninakuchanganya mzee wangu?” nikamuuliza kwa sauti tulivu nikiwa sijui  nililokuwa ndani ya moyo wa mzee huyo..
 
“Mimi ndiye Sharif Nasri. Huyu ni  binti  yangu na alishakufa miaka mitano iliyopita!”
 
Kauli ya yule mzee ikanishitua na mimi.
  
“Umesema alishakufa miaka mitano iliyopita?” nikamuuliza.
 
“Ndiyo alishakufa. Hivi sasa ni marehemu. Uliponiambia ni huyu umenichanganya sana”
 
“Kama alishakufa miaka mitano iliyopita, mbona nimemuona na ameniambia nije kumuulizia hapa?”
 
Nikaona mama mmoja na binti mmoja aliyekuwa amefanana na Ummy, wakitoka pale barazani. Pengine ni baada ya kusikia yale maneno.
 
“Kuna nini?” Yule mama akauliza.
 
SASA ENDELEA
 
“Huyu kijana amekuja na habari za kushangaza kidogo” Yule mzee alianza kumueleza.
 
“Kwani yeye ni nani?”
 
“Sikiliza nikueleze. Yeye amekuja kumuulizia Ummy”
 
Yule mama akanitazama kisha akaurudisha uso wake kwa yule mzee.
 
“Yeye hajui kama Ummy hivi sasa ni marehemu?  Amekuja kutukumbushia msiba tuliokwishausahau”
 
“Anasema alikutana naye na alimuagiza aje hapa nyumbani!”
 
“Alikutana naye lini?” Yule mama aliuliza kwa mshituko.
 
“Eti  mlikutana llini??” Yule mzee akaniuliza.
 
“Nilikkutana naye jana na leo niliongea naye asubuhi kwa simu” nikamjibu.
 
Mama akatikisa kichwa.
 
“Huyo siye Ummy. Ummy alikwishakufa mmika mitano iliyopita” Mama alisema.
 
“Nimemuonesha hii picha ya marehemu. Ameniambia Ummy aliyekutana naye ndiye huyo”
 
“Haiwezekani. Huyo aliyekutana naye si Ummy”
 
Yule msichana  aliyetokana yule mama akanitazama.
 
“Umesema uliongea naye kwenye simu leo?” akaniuliza.
 
“Ndiyo niliongea naye”
 
“Ulimpigia au alikupigia?”
 
“Alinipigia yeye”
 
“Hebu tuoneshe namba  yake”
 
Nikatoa simu yangu na kuitafuta namba aliyonipigia  yule msichana, nikamuonesha.
 
Msichana aliisoma ile  namba kisha akagutuka.
 
“Mama hii ndiyo iliyokuwa namba ya marehemu dada!” akasema kwa sauti ya  kutaharuki.
 
“Kwani unaikumbuka vizuri?”Yule mama akamuuliza.
 
“Naikumbuka” Msichana alisema na kurudia kuitaja ile namba kwa kuikariri  kisha  akaongeza.
 
“Ni namba ya marehemu kweli”
 
Nyuso za watu wote watatu zikawa zimebadilika. Nilijuta kufika pale nyumbani na kukuta niliyoyakuta.
 
“Hebu tueleze vizuri unajuana naye vipi huyu Ummy?” Yule  mama akaniuliza.
 
Ikanibidi nieleze ukweli wote tangu  babu yangu alipofariki mpaka nikaenda  katiika nchi nilizokwenda kufuatilia madeni ya babu. Nikaeleza jinsi msichana huyo  alivyowaua watu niliowafuata katika kila nchi niliyokwenda. Na mtu wa mwisho aalimuua Dar es  Salaam mara tu niliporudi kutoka Afrika Kusini.
 
Niliwaeleza kwamba  niliporudi nilimuona  huyo msichana akishuka kwenye ndege akiwa amefuatana na mtu mmoja.
 
“Niliwafuatilia hadi Mbezi ambako niliona wakiingia  katika nyumba  moja. Siku ya piili yake nikaona kwenye vyomba vya  habari yule mtu ameuawa na alikuwa ni mmoja wa watu waliokuwa wanadaiwa na  babu yangu”
 
Mama alitoa mguno mzito akamtazama yule binti kisha akamtazama yule mzee ambaye nilikwisahisi kuwa alikuwa mume wake.
 
“Huyu kijana amekuja na habari kubwa” akawambia kisha akanitazama na kuniuliza.
 
“Sasa mlikutana wapi na huyu msichana mkiwa hapa Dar”
 
“Tulikutana jana. Sijui alipataje namba yangu akanipigia simu…”
 
“Wewe ulijuaje kuwa ni yeye aliyekupigia simu?”
 
“Sikujua kama alikuwa yeye. Aliniambia nimfuate katika  hoteli moja pale Masaki, akaniambia alikuwa na taarifa kuhusu mali za babu yangu. Nikafika  hapo hoteli. Nikaingia  katiika chumba alichoniambia ananisubiri.
 
“Nilipoingia humo chumbani nikamuona yeye. Kwa vile nilivyojua kuwa ndiye aliyeua wale watu, nilidhani alitaka  kuniua na mimi nikatoka mbio bila kumsikiliza. Niliporudi nyumbani alinipigia simu akaniuliza kwanini nilimkimbia”
 
Niliendelea kuwaeleza jinsi nilivyojibizanana na msichana  huyo hadi akanitajia jina lake na ubinti wake na akanitaka nifike nyumbani kwao Mwananyamala ili  nionane naye.
 
“Namba  ya nyumba hii alikutajia  yeye?” 
 
“Ndiyo alinitajia yeye. Jana sikufika. Leo asubuhi akanipigia simu na  kunisisitiza kuwa nifike kumuulizia. Ndio nikafika  na kukutana na  huyu mzee  hapa”
 
Palipita kimya cha karibu robo dakika. Wenyeji wangu hao walikuwa wameduwaa wakinitazama. Sikuweza kujua walikuwa wananiwazia nini.
 
Nikahisi kijasho chembamba kikinitiririka kwenye mfereji  wa  uti wa mgongo wangu.
 
Nilikuwa nikijiuliza kama ule ulioua watu Botswana, Zimbabwe na Afrika Kusini uulikuwa ni mzuka wa Ummy na kwamba nilikutana na kuzungumza na  mzuka?
 
Maswali hayo yalikuwa yakipita akilini mwangu kimya kimya huku nikikabiliwa na kazi  ya kukwepa macho ya wale wazee waliokuwa wakinitazama.
 
Ni vyema niseme ukweli kwamba wakati ule tunazungumza, miguu yangu ilikuwa inatetemeka kwa  hofu.
ITAENDELEA kesho hapahapa Usikose uhondo huu

No comments:

Post a Comment