Thursday, April 13, 2017

UCHAGUZI MDOGO TANGA PRESS CLUB WAPATA VIONGOZI KUJAZA NAFASI ZILIZOKUWA WAZI.



Tanga, WAJUMBE wa mkutano mkuu maalumu wa uchaguzi wa Tanga Press Club (TPC) imewachagua viongozi wa nafasi ya makamo mwenyekiti na katibu msaidizi nafasi ambazo zilikuwa wazi.
Akizungumza mara baada ya kuchaguliwa, Makamo mwenyekiti, Lulu George, aliwataka waandishi wa habari kujiendeleza kielimu ili kuifanya taaluma yao kwa weledi.
Alisema waandishi wengi wamekuwa wakibweteka kwa kiwango walichonacho  na kusahau kuwa taaluma ya uandishi wa habari inakuwa kila siku.
“Nawashukuru kwa kunichagua kwa kura zote bila kupingwa hata kura moja, hii inaonekana muko na imani name na niwahakikishieni nitasimamia haki zenu na maendeleo ya umoja wetu” alisema George na kuongeza
“Lakini nikumbushie kitu kimoja ambacho ni muhimu tuondosheni makundi na kuwa kitu kimoja kila mmoja ajione sawa na mwenzake” alisema
Kwa upande wake, Katibu msaidizi, Alexsander Abraham, aliepata kura 14 kati ya 15  alisema anaomba ushirikiano ili kuweza kuienua klabu hiyo.
Alisema   atatoa ushirikiano na kuleta umoja na kuwahakikishia wanachama  kuwa atasimamia haki na maslahi yao ndani ya klabu na katika uandishi wao.
                                            


Katibu wa Tanga Press Club (TPC) Anna Makange, akisoma taarifa ya klabu wakati wa mkutano wa marekebisho ya Katiba na kabla ya uchaguzi mdogo wa kuziba nafasi ya makamo mwenyekiti na Katibu Msaidizi mkutano uliofanyika  ukumbi wa klabu hiyo  juzi.

 Wajumbe wa mkutano wa Marekebisho ya Katiba ya Tanga Press Club (TPC) pamoja na wasimamizi wa uchaguzi mdogo wa kujaza  nafasi ya Makamo Mwenyekiti na Katibu Msaidizi wa klabu hiyo wakipitia mistari ya Katiba ya Klabu  kabla ya kufanyika uchaguzi juzi.



No comments:

Post a Comment