Wednesday, April 19, 2017

SIMULIZI, NILIKIONA CHA MOTO URITHI WA BABU SEHEMU YA 12

ZULIA LA FAKI
 
NILIKIONA CHA MTO URITHI WA BABU 12
 
ILIPOISHIA
 
Vile vile nilitaka  kujua jinsi yule msichana anavyohusika  na mali za babu yangu.  Amejuaje kama mali za babu yangu zimepotea?
 
Au ana maelezo gani ambayo anataka kunipa kuhusu mali hizo na ameyapata wapi?
 
Suala la mali lilinipa shauku lakini suala la mauaji lilinitia  hofu.  Ilibidi nigwaye na nifikiri vya kutosha kabla ya kuamua kwenda huko Mwananyamala.
 
Baada ya kuwaza kwa muda mrefu nilitoka pale nyumbani, nikaenda  kwenye mkahawa uliokuwa jirani. Niliagiza chakula nikala huku nikiwaza.
 
Nilipomaliza kula niliitoka. Siku ile kulikuwa na mechi kati ya Simba  na Yanga. Nikaenda uwanja wa taifa. Nilikuwa mpenzi  wa mpira wa miguu na shabiki wa moja ya timu hizo.
 
Niliangalia mpira hadi saa kumi na mbili jioni. Sikupata furaha kwa vile timu zilitoka sare bila  kufungana. Nikarudi nyumbani.
 
Mpaka muda huo nilikuwa nimepuuza kwenda Mwananyamala kumuulizia  Sharif Nasri.
 
Asubuhi ya siku ya pili yake yule msichana akanipigia simu.
 
“Mbona hukwenda kule nilikokuelekeza?” akaniuliza.
 
“Nitakwenda leo”
 
“Ni muhimu. Tafadhali usipuuze”
 
SASA ENDELEA
 
Baada ya kunywa chai niliona niende huko Mwananyamala alikonielekeza huyo msichana ili nikapate taarifa zake. Nilitarajia si tu ningeweza kugundua  msichana huyo alikuwa nani pia ningeweza kujua sababu ya kuwaua wale watu.
 
Hata hivyo  wakati  nikienda huko Mwananyamala  nilikuwa nikijua fika kwamba yule msichana alikuwa mtu wa hatari.
 
Lakini kubwa zaidi lililonisukuma niende, ni vile alivyoniambia  kuwa alikuwa na  tarifa ya malli za babu yangu ambazo mpaka muda ule zilikuwa ni kitendawili nilichoshindwa kukitegua.
 
Kadhalika mauaji yale ya watu wanne ambao  walikuwa wakidaiwa na babu yangu yalizidi kunipa shauku ya kutaka kumjua vyema msichana  huyo ambaye mpaka muda ule  nilikuwa nikiamini kwamba ndiye aliyewaua.
 
Nilipofika Mwananyamala niliutafuta mtaa niioelekezwa hadi nikaupata.  Nikaitafuta nyumba  yenye namba aliyonitajia yule  msichana. Nilipoiona nilijisikia kuanza kupata hofu nikajiambia kuwa nami leo naenda kufa.
 
Sikujua ni kwanini nilipata  hofu. Lakini nilihisi nilipata hofu kwa sababu nilipagundua mahali ambapo ningepata taarifa za yule msichana ambazo zilikuwa zikiumiza kichwa changu.
 
Mbele ya ile nyumba nilikuta mzee aliyekuwa amekaa kwenye kiti cha uvivu akivuta mtemba.
 
Alikuwa mzee mrefu na mwembamba aliyekuwa na ndevu nyingi nyeupe. Alikuwa amevaa shati jeupe na suruali nyeupe. Kichwani alikuwa amevaa kofia ya darize.
 
Jinsi nilivyomsoma kutokana na mavazi yake na sura yake, alikuwa mswahili wa pwani aliyekuwa amechanganya na ushirazi. Umri wa mzee huyo haukuwa chini ya miaka sabini na mitano ingawa bado alionekana kuwa na nguvu za kutosha.
 
Nilisimamisha gari karibu na baraza ya nyumba hiyo nikaizima moto na kutoa gea zote na kuvuta hand break  na kushuka.
 
Vile nilivyomuuona  mswahili nikamtolea salaam.
 
“Asalaam alaykum”
 
“Waalayka salaam” aliniitikia.  Ingawa alikuwa mwembamba, sauti  yake ilikuwa nzito inayokwaruza.
 
“Habari za hapa?” niliendelea kumsalimia nikiwa nimesimama mbele yake.
 
“Nzuri. Karibu” akanikaribisha  huku akinitazama kwa macho ya udadisi.
 
Macho yake yalikuwa madogo  yaliyokuwa na kope nyeupe.
 
“Samahani mzee wangu, kulikuwa na mtu ninamuulizia. Aliniambia  ninaweza kumpata hapa”
 
“Ni nani?”
 
“Anaitwa Ummy Sharif Nasri”
 
Mzee nilipomtajia  jina hilo alishituka akautoa mtemba wake midomoni kisha akaniuliza tena huku akiwa amenikazia macho.
 
“Unasema  nani?”
 
“Ummy Sharif  Nasri”
 
Mzee aliendelea kunikazia macho.
 
“Wewe unatokea wapi?”
 
“Natokea hapa hapa Dar”
 
“Unamfahamuje  Ummy?”
 
“Sikuwa nikimfahamu tangu zamani ila  jana nilipigiwa simu na msichana aliyejitambulisha kwa jina hilo akaniambia nikutane naye kwa sababu ana taarifa za mali za marehemu babu yangu”
 
“Alikwambia  anaitwa Ummy Sharifu Nasri?”
 
“Ndiyo”
 
“Alikuelekeza uje kwenye  nnyumba  hii?”
 
“Ndiyo”
 
“Uliwahi kumuona yeye mwenyewe?”
 
“Nilimuona jana”
 
“Una hakika kwamba ulimuona Ummy?”
 
“Ndiyo nnilimuonna”
 
“Nikikuonesha picha  yake unaweza kumtambua”
 
“Ndiyo  nitamtambua”
 
“Hebu subiri”
 
Mzee alionesha wazi nilimchanganya akili. Aliinuka kwennye kiti akaingia  ndani.
 
Sikujua ni  kwanini alitaharuki.  Baada ya muda  kidogo alitoka akiwa ameshika kitabu cha picha.
 
“Hebu sogea hapa  karibu” akanniambia huku akifungua karasa za kile kitabu.
 
“Hebu angalia hii picha. Msichana uliyemuona ndiye huyo?”
 
Mzee alinionesha picha  moja ya ukubwa wa bahasha ya barua. Ilikuwa ikumuonesha yule  msichana akitabasamu.
 
“Ndiye huyu?” Mzee akaniuliza.
 
“Ndiye yeye”
 
“Mtazame vizuri”
 
“Nimemtazama vizuri, ndiye yeye Ummy Sharif Nasri”
 
“Unaponiambia  hivyo unanichanganya…!”
 
 
ITAENDELEA kesho Usikose nini kitatokea baada ya picha kuonysha Ummy Sharif Nasri ndio yeye.

No comments:

Post a Comment