Friday, April 28, 2017

MWANAMKE ALIEKUWA NA KILO 500 APUNGUA HADI KILO 172

Eman Abd El Aty adaiwa kupunguza uzani kutoka kilo 500 hadi 174 na sasa atasafrishwa hadi UAEMwanamke aliyekuwa na uzani mzito zaidi duniani atasafirishwa hadi katika milki za kiarabu UAE baada ya mzozo kuhusu uzani wake katika hospitali ya India ambapo alikuwa akipatiwa matibabu.
Hospitali ya Saifee mjini Mumbai ilisema kuwa Eman Abd El Aty alifanyiwa upasuaji wa kupunguza uzani na sasa alikuwa huru kuondoka kwa sababu ana uzani wa kilo 172 kutoka kilo 500 alizokuwa nazo awali.
Lakini dadake alimshutumu daktari wa upasuaji huo kwa kudanganya na kumuomba amruhusu dadake aendelee kukaa katika hospitali hiyo.
Kwa sasa ataelekea katika hospitali ya Burjeel huko Abu Dhabi.
Taarifa iliotolewa na daktari wa bi Abd El Aty imesema kuwa atapatiwa matibabu muhimu kwa kuwa hospitali hiyo iko karibu na nyumbani.
Hospitali ya Saifee imeongezea kwamba ilikuwa fahari kwa juhudi zilizofanywa na kundi la madaktari wake ikidai kuwa mgonjwa huyo aliwasili kupitia ndege ya kubebea mizigo na sasa anarudi kama abiri katika ndege ya watu.
Mapema hospitali hiyo ilikuwa imepinga madai kwamba dadake El Aty, Shaimaa Selim ambaye alitoa kanda fupi ya video katika mitandao ya kijamii akidai kwamba dadake aliyekuwa hawezi kuzungumza ama hata kutembea hajapunguza uzani mkubwa kama hospitali hiyo inavyodai.
Daktari wa upasuaji wa watu walionenepa kupitia kiasi Muffi Lakdawala pia alikana madai hayo katika mtandao wa Twitter.

No comments:

Post a Comment