Friday, April 14, 2017

UMUHIMU WA KULA BAMIA

Umuhimu wa kula bamia katika afya

Kwa kibantu huitwa bamia ila kwa kimombo huitwa ladies finger.  Huitwa ladies finger kwa sababu zina mfanano bayana na  vidole vya mwanadamu. Swali la msingi je unapenda bamia? Kama huwa hupendelei kuzitumia naomba uanze kuzitumia kwani zina faida katika afya yako, miongoni mwa faida hizo ni;

1. Inasemekana ni chakula kizuri kwa watu wenye msongo wa mawazo,wanaojisikia uchofu.

2. Ni chakula kizuri kwa wanaotaka kupunguza mwili.

3. Mbegu za bamia zina protine nyingi na mafuta. Ambazo husaidia kuupa mwili nguvu na joto.

4. Inasaidia mmeng'enyo wa chakula na kupata choo vizuri. Kwa wale wenye matatizo ya choo unashariwa kutumia kwa wingi ili kukabiliana na adha hiyo.

5. Madini ya potassium,calcium na magnesium.
mgblog

No comments:

Post a Comment