Wednesday, December 31, 2014

KILIO CHA MAJI , WETE PEMBA

Kumekucha blog

Pemba, WAKAZI wa mji wa Wete Wilaya ya Kaskazini Pemba, wamesema kero ya upatikanaji wa maji safi majumbani haitoisha hadi Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) kukarabati miundombinu yake ambayo imezidi kuwa chakavu.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi nyakati tofauti, wakazi hao wamesema kero ya maji mjini humo imekuwa kero na kushindwa kuwafikia majumbani baada ya njia nyingi za  mabomba yanayopitisha maji  kupasuka.

Wamesema hali hiyo imekuwa ikiwalazimu kwenda mabondeni ambako pia upatikanaji wake umekuwa wa shida baada mabonde mengi kukauka maji kutokana na kiangazi.

“Sisi huku kizimbani maji hayafiki kabisa na tumeshazoea tukiamka tunakimbilia mabondeni---mabomba mengi yamepasuka na maji yanaishia njiani na hili tumelisema sana” alisema Amran Hamis

“Tumetoa taarifa kwa mamlaka yetu ya  maji kama inavyojulikana kwa jina la  zawa----lakini chakushangaza wao pia wanalitambua na kila siku wanatuambia watabadilisha mabomba” alisema

Akizungumzia kwa undani kero hiyo mkazi wa Chasasa, Said Bakar,  alisema wamekuwa katika wakati mgumu kuweza kukabiliana na shida hiyo hasa vipindi vya watoto kwenda shule baada kusongomana katika visima bondeni.

Alisema vipindi vya shule maeneo ya mabondeni watoto wamekuwa wengi na kila mmoja kutaka kuwahi shule na hivyo kusubiria hadi saa 2 jambo ambalo nao wamekuwa wakichelewa kwenda katika majukumu yao kwa wakati.

Aliishauri Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) kuifanyia ukarabati miundombinu yake ili kuweza kupata maji majumbani jambo ambalo maji mengi yamekuwa yakipotea baada ya mabomba kuwa chakavu.

“Nashauri tu mamlaka yetu ikafanya ukarabati taratibu angalau tuweze kupata maji kidogo kidogo vyenginevyo shida hii itatukondesha na kutuchosha” alisema Bakar

Alisema kwa muda mrefu wamekuwa walilalamika na kushindwa kilio chao kupatiwa ufumbuzi na hivyo kusema ni muda muafaka wa sasa kuweza kupatiwa ufumbuzi kwani limekuwa la muda mrefu.

                                         Mwisho

No comments:

Post a Comment