Saturday, December 27, 2014

NDOA YAVUNJIKA ,KISA KIJUBADILISHA AFANANE NA KIM KADARSHAIAN

Ndoa yavunjika, kisa mwanamke amegoma kujibadilisha ili afanane na Kim Kadarshian…


Ndoa yavunjika, kisa mwanamke amegoma kujibadilisha ili afanane na Kim Kadarshian…

Kim-Kardashian-Looking-Back-Side-Face-CloseupsDunia na vioja vingine 2014, eti unaweza kumuacha mpenzi wako kwa kuwa hafani na staa fulani ambaye wewe unampenda?
Mwanamke mmoja ambaye jinalake ni Rahma, kutoka Cairo, Misri, amedai talaka kwa mumewe kwa kuwa amekuwa si mwaminifu, amekuwa akimsaliti mara kwa mara kutokana na kile ambacho mwanamke huyo amekisema eti mumewe anataka mke wake afanane na Kim Kadarshian au muigizaji Haifa Wehbe.
Mara kadhaa mume wa mwanamke huyo amekuwa akimtaka avae na kutengeneza nywele zake ili afananena mmoja ya mastaa hao, alikataa, amesema anatazama mambo mengine ya msingi kuyafanya ikiwemo kumlea mtoto wake wa mwaka mmoja, hivyo asingeweza na hili la kujitengeneza ili afanane na mastaa hao ambao yeye aliwaita midoli wa kwenye TV!
Kim Kadarshian
Kim Kadarshian
Haifa Wehbe, Mwanamitindo, mwanamuziki na muigizaji kutoka Lebanon.
Haifa Wehbe, Mwanamitindo, mwanamuziki na muigizaji kutoka Lebanon.
Kwa kuwa dini ya mwanamke huyo inaongozwa na Sheria ya Shariah ambayo inaruhusu mwanamke kuachika na mahari iliyotolewa kurudishwa, mwanamke alifanya maombi ya kudai talaka ili aendelee na maisha yake mengine.
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,kumekucha blog

No comments:

Post a Comment