Tuesday, December 30, 2014

SETH ROGEN NA JAMES FRANCO WAVUNJA REKODI YA MAUZO YA FILAMU MAREKANI

Kwenye rekodi za mauzo ya filamu za Sony, hii imevunja rekodi ndani ya siku tano tu!

Kwenye rekodi za mauzo ya filamu za Sony, hii imevunja rekodi ndani ya siku tano tu!

The Inter II
Jamaa ambao wamecheza movie hiyo kama waandishi wa Habari, Seth Rogen na James Franco.
Labda nikupe dondoo kidogo kuhusu movie hii, story ilianzia November 22 ambapo system ya computer za Kampuni ya Sony zilivamiwa na watu wasiofahamika na kuvujisha taarifa mbalimbali za siri ikiwemo email za mastaa mbalimbali Duniani, mishahara yao na baadhi ya script za movie zitakazotolewa siku za karibuni.
Movie ya ‘The Interview’ ilivuja pia, story ya movie hii iko hivi; waandishi wawili wa Habari walipata mwaliko kuonana na Rais wa Korea Kaskazini, wanapanga njama na CIA ili wamuue Rais huyo, Kim Jong-un.
Co
Matangazo yaliyowekwa sehemu mbalimbali Marekani kuhusu kuonyeshwa kwa movie hiyo.
Serikali ya Marekani ililaani kitendo cha uvamizi huo kwa kuishutumu Serikali ya Korea Kaskazini kwamba imehusika na uvamizi wa system hiyo, Korea walikanusha huku kikundi cha waliohusika kikipiga mkwara wa kushambulia kumbi zote za sinema Marekani ambako ilipangwa kuonyeshwa movie hiyo, Rais Obama akasema ionyeshwe na hakuna hatari yoyote ya mashambulizi itakayotokea.
Baada ya mvutano huo, siku ya Christmas December 25 iliachiwa rasmi mtandaoni ambapo watu walikuwa na uwezo wa kuidowload na kutazama katika kumbi mbalimbali ilikokuwa ikionyeshwa.
Jamaa aliyecheza kama Rais wa Korea Kaskazini.
Jamaa aliyecheza kama Rais wa Korea Kaskazini.
Baada ya kuanza kuuzwa movie hiyo, Sony wamesema ndani ya siku tatu movie hiyo imefanya mauzo ambayo haikuwahi kutokea siku za nyuma, imeuza zaidi ya dola mil. 18 ndani ya siku tatu, hii ni rekodi ya kipekee haikuwahi kutokea mauzo ya kiasi hiki siku za nyuma.
Hapa kuna trailer ya movie hiyo, unaweza kuitazama mtu wangu.

Hautopitwa na stori yoyote inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,kumekucha blog

No comments:

Post a Comment