Tuesday, August 23, 2016

AMEZA VISI 40 TUMBONI

Mwanamume ameza visu 40 nchini India

Visu vilivyotolewa tumboniMadaktari katika mji wa Amritsar kaskazini mwa India wamesema, wametoa visu 40 kutoka kwa tumbo la mwanamume mmoja.
Mwanamume huyo ambaye hakutajwa jina lake mwenye umri wa miaka 42 alikuwa amevimeza visu hivyo kwa muda wa miezi mitatu.
Daktari Jatinder Malholtra, ameambia BBC kwamba alikutana na mwanamume huyo wiki iliyopita alipokuwa akihisi maumivu makali kwenye tumbo lake.
Alisema mwanamume huyo hakuwafahamisha madaktari hao kwamba alikuwa akimeza visu.

No comments:

Post a Comment