Monday, August 15, 2016

MUHONGO, IFIKAPO 2020, UMEME NCHI NZIMA



Tangakumekuchablog
Mlalo, WAZIRI wa Nishati na Madini, Sospeter Muhongo, amesema Serikali imeadhimia usambazaji umeme vijijini (Rea) kuhakikisha shule, hospitali na vituo vya afya vinakuwa na umeme lengo likiwa ni kuondosha kero na kuongeza ufanisi.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara jana, Muhongo alisema Serikali inatambua kero ya wanafunzi kukosa huduma ya umeme pamoja na vituo vya afya hasa nyakati z ausiku.
Alisema shule zote za mjini na vijijini pamoja na zahanati ifikapo mwaka 2020 ziwe zinatumia umeme na kuondokana na kutumia mishumaa jambo ambalo ni hatari kiafya na usalama.
“Serikali haitaki kuona wanafunzi wanatumia mishumaa kujisomea usiku, vilevile pamoja a vituo vya zahanati madaktari na manesi kutumia tochi mfumo huo uwe mwisho” alisema M,uhongo na kuongeza
“Kama umeme umeshafika hadi vijijini kuna sababu gani shule na vituo vya afya visiwe na umeme ilhali nguzo zinapita juu ya majengo yao” alisema
Akizungumza katika muktano huo, Mbunge wa jimbo la Mlalo, Rashid Shangazi, amelitaka Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Mkoa wa Tanga kuwaekea ofisi ya kupokea taarifa na malalamiko  katika kila  jimbo ya majimbo ya Lushoto.
Alisema kwa sasa wateja wa umeme wamekuwa wakisafiri zaidi ya kilometa 80 kwenda Lushoto kupata huduma ya umeme jambo ambalo wananchi limewachosha hivyo kutaka kuangalia kwa jicho la pili.
Alisema kuwepo kwa umeme mashuleni kutaweza kuwa msaada kwa wanafunzi kujisomea ikiwa na pamoja na kuongeza uelewa pampja na kuondosha alama sifuri shule.
                                                      Mwisho





Kwa habari, matukio na michezo ni hap[ahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment