Wednesday, August 17, 2016

WAFANYAKAZI WANNE WAFUKUZWA KAZI KWA UNENE MISRI

Wafanyakazi nane wafukuzwa kazi kisa unene

Habari hii imeripotiwa na BBC ambapo imetokea nchini Misri kwenye television ya Taifa hilo ambapo imewafukuza kazi wafanyakazi 8 wa kike na kuwashauri waende wakapunguze uzito wa mwili.
Chama cha Radio na Televisheni nchini Misri ( ERTU) kimewapa wanawake hao muda wa mwezi mmoja kupunguza uzito kabla ya kuruhusiwa kuonekana tena kwenye television.
BBC
Tangazo hilo limezua lawama kutoka kwa watangazaji walioathiriwa ambapo mmoja wao Khadija Khattab, mtangazaji wa kituo cha Channel 2, amesema kuwa anataka watu ndio watazame kipindi chake na waamue wenyewe ikiwa ana uzito wa juu.

No comments:

Post a Comment