Tuesday, May 9, 2017

BNTI WA KIMISRI ALIE NA UZITO MKUBWA DUNIANI ADAIWA KUUGUA UGONJWA WA MOYO

Madaktari wa Abu Dhabi sasa wanasema kuwa bi Eman Abd anaugua magonjwa tofautiMwanamke wa Misri aliyeaminika kuwa mtu mzito zaidi duniani sasa anatibiwa matatizo kadhaa ya kiafya katika hospitali moja ya Abu Dhabi.
Eman Abd El Aty aliyedaiwa kuwa na uzani wa kilo 500 aliondoka katika hospitali moja ya India wiki iliopita baada ya madaktari kusema kuwa alipoteza zaidi ya takriban kilo 250.
Lakini madaktari huko UAE sasa wanasema anaugua magonjwa ya moyo pamoja na vidonda vilivyosababishwa na kulalalia kitanda kwa muda mrefu mbali na uzito wake wa kupita kiasi.
Katika majuma ya hivi majuzi ugomvi ulizuka kati ya madaktari nchini Idnia na familia yake.
Ulianza baada ya dadaake ,Shaimaa Selim kutoa kanda fupi ya video katika mitandao ya kijamii akidai kwamba dadaake alikuwa hawezi kuzungumza na hata kutembea kinyume na ilivyodaiwa na hospitali hiyo.
BBC

No comments:

Post a Comment