Thursday, May 11, 2017

SIMULIZI, NILIKIONA CHA MOTO URITHI WA BABU SEHEMU YA 25

Zulia la faki 0655 340572
 
NILIKIONA CHA MTO URITHI WA BABU 25
 
ILIPOISHIA
 
“Nimelikuballi hilo wazo. Kwa hiyo atakaponipigia simu nitazungumza naye baada ya hapo nitakujulisha”
 
“Utakapotujuliasha, tutafika  mahali hapo haraka sana”
 
“Sawa. Inspekata”
 
Baada ya kuagana na Inspekta huyo  niliondoka hapo kituo cha polisi na kurudi nyumbani. Kwa sababu ya yale mawazo ya Ummy kukaa kichwani mwangu wakati wote, nilikuwa sipendi kutembea zaidi ya kukaa nyumbani kwangu.
 
Kwa sababu ya kiherehere, nilipofika  nyumbani nikampigia mimi. Simu ya Ummy haikupatikana. Siku ile nilijaribbu kumpigia mara  kadhaa lakini simu yake ilikuwa haipatikani.
 
Jioni yake Inspekta Amour alinipigia simu akaniuliza kama Ummy alinipigia.
 
“Hajanipigia bado”  nikamjibu.
 
“Na wewe umejaribu kumpigia?”
 
“Nimejaribu mara nyingi lakini simu yake  haipatikani”
 
SASA ENDELEA
 
“Sawa. Tuendeleaa kusubiri. Ninaamini kuna  wakati atakupigia au wewe utapiga na utampata”
 
“Kunipigia ni laziama. Mara nyingi hunishitukizia”
 
“Hata kama atakupigia usiku wa manane, pangana naye mahali pa  kukutana halafu  nipigie muda huo huo”
 
“Sawa Inspekta”
 
Inspekta huyo akakata simu. Mpango huo wa polisi ulikuwa umenipa  matumaini. Mwanzo nilikuwa sitaki yule msichana anipigie simu lakini baada ya polisi kuandaa mpango huo nilikuwa na hamu ya kuona Ummy ananipigia simu.
 
Kila nilipopigiwa simu na mtu mwingine nilikuwa nashituka nikidhani ilikuwa simu ya Ummy. Wakati wote simu yangu ilikuwa mkononi ili iwe rahisi kuisikia inapopigwa.
 
Usiku ule  uukapita bila kupigiwa simu na Ummy. Siku iliyofuata nayo ikapita. Usiku wake Inspekta Amour alinipigia tena kuniuliza. Nilifurahi alivyokuwa ananipigia kwani alikuwa ananipa  moyo sana.
 
“Hajapiga bado?” akaniuliiza.
 
“Hajapiga lakini ninaamini kwamba atapiga”
 
“Sawa. Tuendelee kusubiri”
 
Asubuhi ya siku ya tatu yake nikaamshwa usingizini na mlio wa simu. Niliamka nikaishika simu yangu ambayo nilikuwa nikiiweka mchagoni mwa kitanda ili iinapoita niweze kuisikia.
 
Nikayafikicha macho yangu kuondoa ukungu  wa usingizi  kisha nikaitazama sikrini ya simu.
 
Alikuwa ni Ummy!  Moyo ukanishituka. Nikainuka na kukaa  kitandani kasha nikaipokea ile simu.
 
“Hello!” Nikasema kwa sauti iliyoonesha wazi kuwa nilitoka  usingizini.
 
“Natumaini umzima?” Sauti ya Ummy ikasikika kwenye simu.
 
“Mimi mzima, sijui  wewe”
 
“Mimi mzima tu.  Mbona upo kimya?”
 
“Nimekupigia mara nyingi lakini hupatikani”
 
“Si wakati wote ninaweza kupatikana”
 
“Nimeshaamua kuwa tuukutane mahali popote”
 
“Kwanini mmekwenda kufukua kaburi langu?”
 
Moyo wangu ukapiga kwa kishindo.
 
“Kaburi lako?” Nikamuuliza kwa kubabaika.
 
“Mmelifukua juzi na kuutoa mwili wangu!”
 
Moyo uliendelea kunipiga kwa nguvu.
 
Akilini mwangu nilijiambia, huu kweli ni mzuka.  Amejuaje kuwa tulifukua kaburi lake?
 
Nikajiuliza tena kama itakuwa busara kukubali kukutana  naye.
 
Mawazo ya kukutana na msichana huyo yalinibadilika hapo hapo. Kwa kweli nisingeweza kukaa na kuongea na mtu aliyekwisha kufa.
 
“Kwa kweli sikufurahi” Sauti ya Ummy iliendelea  kuniambia baada ya mimi kuwa kimya.
 
Kikapita kimya kingine kabla ya sauti hiyo kusikika tena.
 
“Umesema tukutane wapi?”
 
Ilinichukua muda kumjibu.
 
“Sema wewe tukutane wapi”
 
Kwa kweli sauti yangu sasa ilikuwa imenywea. Ujasiri wote ulikuwa umeshanitoka.
 
“Tukutane kule hoteli, Masaki”
 
“Hoteli gani?’
 
“Ile ambayo tulikutana mara ya kwanza”
 
“Kule ni mbali sana. Kwanini tusikutane katika hoteli iliyo  karibu”
 
“Iliyo karibu na wapi?”
 
“Iliyopo hapa katikati ya jiji”
 
“Nadhani Masaki kunafaa zaidi”
 
“Lakini anagalia, usichukue chumba. Tukutane mahali pa wazi”
 
“Mbona  umebadilika?”
 
“Tukutane mahali pa wazi tu kwa ajili ya mazungumzo yetu”
 
“Sawa, nitakufahamisha utanikuta wapi”
 
“Saa ngapi?”
 
“Tufanye saa nne”
 
“Sawa. Utanijulisha”
 
Ummy akakata simu. Hapo hapo nikampigia Inspekata Amour
 
“Yule msichana amenipigia simu sasa hivi” nikamueleza Amour kwa pupa.
 
“Amekwambiaje?”
 
“Kwanza amenilaumu kwamba tulikwenda kufukua  kaburi lake na kuutoa  mwili wake. Ameniambia kwamba hakufurahishwa na jambo hilo”
 
ITAENDELEA kesho hapahapa usikose uhondo huu mwanana
 
 

No comments:

Post a Comment