Saturday, May 27, 2017

SHEIKH WA MKOA WA TANGA AWAASA WAFANYABIASHARA WA NAFAKA



Tanga, SHEIKH wa Mkoa Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata) Tanga Juma Liuchu, amewataka wafanyabiashara wa vyakula masokoni kuacha kupandisha bei za bidhaa kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwa Waislamu.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Liuchu amesema Mwezi wa Ramadhani ni mwezi wa machumo na baraka hivyo kuwataka kumuogopa Mungu ili kuepuka kupata dhambi.
Alisema wafanyabiashara wengi hukitumilia kipindi cha mfungo wa Ramadhani kwa kupandisha bei za vyakula hivyo kuwataka kuacha kufanya hivyo na badala yake kuwapa unafuu wafungaji.
“Niwatake wafanyabiashara masokoni na madukani kuacha kupandisha bei za vyakula, hebu tuogope kuingia katika dhambi na tuwape unafuu wafungaji” alisema Liuchu na kuongeza
“Tamaa za pesa ndogo ndogo tena za muda mfupi zisitutoe katika imani na tukawakomoa wafungaji na hili nitalifikisha katika tume ya kudhibiti bei za bidhaa madukani” alisema
Alisema kipindi hiki cha mfungo wafungaji hutumia futari nyingi za nafaka hivyo kuwaasa wafanyabiashara hao kutumia ubinadamu na kuacha kuwalangua.
Katika masoko makubwa Ngamiani, Mgandini, Uzunguni na Makorora Mwandishi wa habari hizi alitembelea na kujionea bei za bidhaa ikiwemo tambi ilikuwa zikuzwa 2,000, kunde, 2,300, maharage 2,000, sukari 2,500 , nazi 800 na mchele ulikuw aukiuzwa 2,300 hadi 2,500.
                                    Mwisho





No comments:

Post a Comment