Tuesday, May 16, 2017

MAPOROMOKO YA MAWE LUSHOTO FURSA KWA VIJANA NA MAMA NTILIE



Luushoto, KUFUATIA mawe zaidi ya matano kufunga barabara Wilayani Lushoto Mkoani Tanga, fursa nyingi za vijana kujipatia kipato ziomejitokeza ikiwemo kuvusha watu kwa pesa.
Mawe hayo yaliyoanguka usiku wa juzi baada ya mvua kubwa kunyesha barabara haipitiki zaidi ya watembea kwa miguu ambao huongozwa na vijana ili kuepuka kuzama ndani ya tope zilizomeza barabara ambayo iko na  ukubwa zaidi ya kilometa 10.
Vijana hao waliobuni mbinu ya kujipoatia pesa wametengeza njia za magogo na kusimamisha mawe ili watu waweze kukanyaga na kupita jambo ambalo wengi wameliona kuwa ni jambo zuri nyenginevyo maafa zaidi yangeweza kujitokeza.
Abushehe Shembilu amesema kwa siku hujipatia elfu 20,000 kwa kuwatoza wasafiri kwa shilingi 500 kila mmoja japo wengine hutoa 200 hadi 100.
Amesema kutokana na wingi wa maeneo ambayo ni hatarishi kila mmoja yuko na kiwango chake kutokana na eneo lake jinsi lilivyo hatarishi ambapo amedai kituo chake ndio kibaya zaidi.
Amesema kuna vijana wengi ambao kuanzia asubuhi hadi usku wamekuwa wakiwabebea mizigo kichwani na kuwafikishia jiwe la mwisho amedai hao ndio wanaoingiza kipato kikubwa.
Shembilu amesema kutokana na kuwa hiyo ni kazi hajali kutapakaa matope  mwili nzima ambapo ifikapo saa sita usiku hufunga kazi yeye na wenzake .
Kwa upande wa mama ntilie wajasiriamali hao wamekuwa wakiuza chakula zaidi ya kilo kumi wali pamoja na ugali na huisha na wateja wakiwa katika foleni ya kutaka chakula.
Asha Abrahman alie katika jiwe la pili lililofunga barabara amesema ametoka Lushoto mjini kupiga kambi hapo na kusema kuwa biashara inaenda vizuri na kuwa na matumaini ya adha hiyo itakapoisha ataweza kupunguza matatizo ya nyumbani kwake.
“Mbali ya kuuza chakula chetu hapa katika jiwe la pili ya maporomoko haya tumekuwa tukiuza chai na chakula kwa watu wanaoelekea Lushoto na wengi wamekuwa wakiishia hapa kwa kuogopa kuruka viunzi” alisema Asha
Alisema kwa jinsi hali ilivyo mbaya uwezekano wa kuondoshwa mawe hayo inaweza kuchukua zaidi ya wiki mbili kutegemeana na mvua kuacha kunyesha.
Amesema endapo mvua itaendelea kunyesha maji kuacha kuporomoko kutoka milimani baada ya wiki moja njia itaanza kupitika na kusema adha hiyo imekuwa fursa kwa wajasiriamali na vijana wanaojituma.

No comments:

Post a Comment