Thursday, May 11, 2017

CHINA YAPELEKA BINADAMU KUISHI MUDA MREFU MWEZINI

Mwaka 2016, wana anga wa China Jin Haipeng (kulia) na Chen Dong walikaa siku 30 anga za juuChina imepiga hatua nyingine katika mpango wake wa anga za juu, baada ya kuanza kufanyia majaribio mpango wa kupeleka binadamu wakaishi kwa muda mrefu kwenye Mwezi.
Wanafunzi wa sayansi wamehamia katika chumba maalum chenye mazingira yanayofanana na ya Mwezi ambapo watakaa kwa siku 200.
Lengo ni kuwaanda kwa safari ya kuishi kwa muda mrefu kwenye kituo cha anga za juu kwenye Mwezi, bila kupokea usaidizi wowote kutoka ardhini.
China imewekeza pesa nyingi sana katika mpango wake wa anga za juu, ikilenga kushindana na Marekani an urusi.

No comments:

Post a Comment